Mkurugenzi wa mfuko wa jamii wa LAPF Eliud Sanda katikati akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na mkutano wao watano wa wadau wa mfuko huo wa jamii unaotarajiwa kuanza kesho katika ukumbi wa mikutano wa AICC jijini arusha wa kwanza kulia ni mkutugenzi wa wa huduma kwa wanachama Valerian Mablangeti (picha zote na woinde shizza,Arusha. Picha na Habari na  Woinde Shizza wa Globu ya Jamii, Arusha


ZAIDI  ya wanachama 400 wa mfuko wa jamii wa LAPF pamoja na wadau mbalimbali wa mfuko huo wanatarajiwa kuuthuria mkutano wa tano wa mfuko huo unatarajiwa kufanyika jijiji Arusha .

Akiongea na waandishi wa habari mkurugenzi wa mfuko huo Eliud Sanga alisema kuwa mkutano huo ni watano kufanyika tangu kuanzishwa kwa mfuko huo na hii ni mara ya kwanza kufanyika jijini Arusha.

Alibainisha kuwa  zaidi ya wanachama 400 wanatarajiwa kushiriki mkutano huu pamoja na wadau mbalimbali wa mifuko ya jamii wakiwemo wa ndani ya nchi pamoja na nje ya nchi huku akibainisha nchi mbalimbali zinazoshiriki mkutano huu  ni pamojna na wadau wa mifuko ya jamii kutoka nchi za zilizopo katika jumuiya ya Afrika mashariki ambapo alitaja kuwa ni pamoja na kenya ,uganda ,burundi  Rwanda na zambia.

Alisema kuwa kwa Apa watu wengine ambao watashiriki na wamealikwa katika mkutano huu ni pamoja na shirika la nyumba tanzania halimashauri  vingozi wa halimashauri zote hapa nchini ,meya wa halmashari zote ,makatibu tawala  pamoja na mifuko mingine ya kijamii.

Alisema kuwa katika mkutano huu kutakuwa na mada mbalimbali ambazo zitajadiliwa na washiriki ikiwemo mchango wa mifuko hii ya hifadhi ya jamii, Nafasi ya mufuko wa jamii ,kujiandaa kustaafu pamoja na kuwapa washiriki elimu kuhusiana na ugonjwa wa saratani.

Alisema leongo la mkutano huu ni kupanua wigo wa maoni pamoja na mawazo ya wananchama huku akibainisha kuwa kauli mbiu ya mkutano huu kwa mwaka hu ni hifadhi ya jamii na ukuaji wa uchumi,

Alisema kuwa mkutano huu utafanyika kwa siku mbili ambapo alibainisha kuwa unatarajiw akufunguliwa na waziri wa tamisemi ofisi ya waziri mkuu na kufungwa na rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...