Timu ya Elimu Sports Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imepokelewa leo na Kaimu Katibu Mkuu Bw. Salum Mnjagila,viongozi wengine wa wizara na wafanyakazi baada ya kuwika katika mashindano ya SHIMIWI mwaka huu yaliyomalizika Jumamosi mjini Morogoro. Timu ya soka ya Elimu Sports imetawazwa mabingwa baada ya kuichapa National Audit, aidha, timu ya Riadha ya wizara imekuwa mshindi wa jumla wa mchezo huo na imenyakua ushindi wa pili katika mchezo wa Darts.
Kaimu Katibu Mkuu Bw. Salum Mnjagila akipokea kombe la ubingwa wa mpira wa miguu katika mashindano ya SHIMIWI mwaka huu
Wafanyakazi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wakifurahia vikombe vya ushindi walivyovipata
Picha ya pamoja ya viongozi wa wizara na wanamichezo wa Elimu Sports. Picha na habari na ntambi bunyazu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...