Mhe. Hamad Rashid Mohamed akitoka katika mkutano na Mwenyekiti wa kamati ya maswala ya Ulinzi na Usalama wa kimatifa Mhe. Saber Chowdury kutoka Bangladesh mara baada ya mjadala huo. Mbunge huyo wa Tanzania ambaye pia ni
Mjumbe wa Mkutano wa Chama cha Mabunge Duniani ameteuliwa na kamati tendaji ya chama cha Mabunge duniani (IPU) kuwa mjumbe wa
kamati ndogo ya ukaguzi wa ndani kwa mahesabu ya mwaka 2013 ya chama hicho.
Uteuzi huo ulifuatia pendekezo la
umoja wa Mabunge ya Afrika lililowasilishwa na katibu mkuu wake Koffi N’Zi
tarehe 22 Oktoba, 2012 kufuatia kikao cha wajumbe wa umoja wa Mabunge ya Afrika
kumchagua Mhe. Hamad kuwakilisha Afrika kuwania pendekezo hilo mbele ya kamati
tendaji ya chama hicho.
Mhe. Hamad Rashid Mohamed akitoka katika mkutano na Mwenyekiti wa kamati ya maswala ya Ulinzi na Usalama wa kimatifa Mhe. Saber Chowdury kutoka Bangladesh mara baada ya mjadala huo
![]() |
Mbunge kijana kutoka Afrika Kusini Mhe. Judith Tshabalala akichangia kwa hisia kali tatizo la ajira kwa vijana na jinsi mabunge mengi duniani ambavyo hayajalivalia njuga swala hili:
|
Mjumbe wa Tanzania katika mjadala wa Wabunge Vijana kujadili na namna ya kupunguza ajira kwa vijana hususani katika kipindi hiki cha uchumi wa utandawazi uliondoandaliwa na Chama cha Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) katika Mkutano wake Mjini Quebec, Canada, Mhe David Kafulila akinyoosha karatasi kupeleka ujumbe wa kuchangia katika mjadala huo.


.jpg)
.jpg)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...