Katika toleo ya Jumatatu wiki hii la Globu ya Jamii na blogu nyingine ilitolewa habari iliyokuwa na kichwa cha ‘TANZANIA KUONDOKA KATIKA KUNDI LA NCHI MASKINI IFIKAPO 2015’
Habari ile ilikuwa na kosa la kiuandishi kwenye eneo la mwaka, ukweli ilikuwa isomeke Tanzania inatarajiwa kuondoka kwenye kundi la nchi maskini na kuwa nchi yenye Uchumi wa Kati ( Middle Income Country) ifikapo mwaka2025 na si 2015.
Mwandishi wa habari ile na ambayo ilimnukuu Naibu Katibu Mkuu Mtendaji Ofisi ya Rais Kamisheni ya Tume ya Mipango, Bw. Clinfford K. Tandari (pichani juu) anachukua fursa hii kumwomba radhi Mhusika Mkuu wa habari ile kwa usumbufu wowote alioupata na pia anawaomba radhi wadau wengine ambao kwa namna moja ama nyingine walikwazika.


will all those angry, rightfully so, commentors be apologizing?
ReplyDeleteKuna waziri wetu Hon Philipo Augustino Mulugo, Dep Min of Education & Voc Training nae aliitangaza Zimbabwe kuwa imo katika muungano wa Tanzania inabidi nae tupate sahihisho lake hapa. Angalia hotuba yake hapa http://www.youtube.com/watch?v=e3BNegmIUKM&feature=share
ReplyDelete