TUNAPENDA KUWAFAHAMISHA WASAFIRI WETU WA RELI YA KATI DARAJA LA TATU KWAMBA, KUANZIA SASA WATOTO WA UMRI CHINI YA MIAKA SABA WATASAFIRI BURE NA WATAPEWA KITI/VITI.
WATOTO HAO WATATAKIWA KUSAFIRI NA WAZAZI/WALEZI WAO NA PIA WAJE NA VYETI VYA KUZALIWA AU BARUA YA SERIKALI YA MTAA HUSIKA KUTHIBITISHA UHUSIANO NA MZAZI/MLEZI WAKE.
MZAZI/MLEZI ATAKAYESAFIRI NA WATOTO HAO ATARUHUSIWA WATOTO WASIOZIDI WAWILI KWA WAKATI MMOJA NA NILAZIMA AJE NA VITHIBITISHO HIVYO WAKATI WA KUNUNUA TIKETI YAKE NA AWAANDIKISHE KWA KARANI/STESHENI MASTA ILI WAWEZE KUPATA TIKETI ZA KUSAFIRIA.
MTOTO ATAKAYEKUTWA NDANI YA TRENI BILA TIKETI ATALIPIA NUSU NAULI YA MTU MZIMA.
TUNAOMBA USHIRIKIANO WENU ILI KUBORESHA HUDUMA HII.
Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa TRL
Mtendaji
Mhandisi Kipallo A.Kisamfu
Dar es Salaam.
Vizuri, wapate viti kwa uhakika, na wakilaghaiwa ama kutishwa ili wapishe viti hatua kali zichukuliwe dhidi ya mafedhuli watakaofanya hivyo.
ReplyDeleteNikiwa mdogo huko mikoani nilisafiri kwa tabu na mateso sana sana. Mtoto wa miaka saba ama nane unatoka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine unaambiwa upishe kiti! Na mtu mzima, bila ya aibu, anakaa na kukutazama tu ukiwa unang'ang'ania kutafuta sehemu ya kushika ili usianguke maana juu hufikii na watu wamejaa.
SiKILIZENI KWA MAKINI NA HIZO TICKET MNAZOAHIDI MSIPOZITOWA TUTAKUJA KULALAMIKA HUMU HUMU KAMA MNAVYOJIJENGEA SIFA HUMU ALAFU AHADI AZITIMII.
ReplyDeletemimi sijapenda je kama unawatoto watano huwezi kusafiri kwasababu sheria ni watoto wawili hii kali rekebisheni hichi.
ReplyDelete