Wachezaji wa timu ya  mpira wa pete wa timu ya Bunge wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania (waliovaa nyeusi) wakicheza  na timu ya chuo cha Ufundi cha Arusha katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid timu  ya Bunge iliibuka mshindi kwa mabao  24 -13
Timu ya  mpira wa pete wa timu ya Bunge wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania (waliovaa nyeusi) wakicheza mpira na timu ya chuo cha Ufundi cha Arusha
Timu ya bunge la jumuiya ya afrika mashariki ikipewa mawaidha na kocha wake Rashid  wakati wa mapunziko 


Picha na habari na Woinde Shizza 
wa Globu ya Jamii

Timu  ya  Bunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania(Bunge sports club) imeweka  kambi ya  wiki mbili  Jijini   Arusha kwa ajili ya mashindano  kombe la Jumuiya  ya Afrika Mashariki yatakayo timua vumbi jijini Nairobi nchini Kenya.

Mwenyekiti  timu  hiyo  ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Kinondoni Idd Azan alisema kuwa pamoja na majukumu waliyonayo bado wana nafasi kubwa  ya kushiriki miashindano hayo na kuhakiksha kuwa kombe hilo linarudi Tanzania.

Azan alisema kuwa lengo la michuano hiyo ni kushirikiana na wabunge wa nchi nyingine zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kudumisha umoja na kuwa na mshikamano kupitia michezo.

Aidha alieleza kuwa lengo lingine ni kudumisha  ushirikiano wa Afrika Mashariki ikiwa ni pamoja na kuwapa burudani wananchi wa  nchi zinazounda Jumuiya husika.

‘’Timu yetu ipo katika hali nzuri na tayari tumeshafanya marekebisho ya makosa tuiyofanya kipindi cha nyuma hivyo watanzania watarajie ushindi kwa kuwa wachezaji wote wapo katika hali nzuri.”alisema Azan

Katika michezo ya kujipima nguvu, timu ya mpira wa pete ya wabunge imeichapa timu ya arusha technical magoli 24-13 katika mtinange uliochezwa katika dimba la Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha.

Katika mtanange mwingine timu ya mpira wa pete ya Ngorongoro creater imechapwa magoli 42-31 na timu ya Mpira wa pete ya Bunge  jijini Arusha.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...