Hayati Mhashamu Aloysius Balina


Imeandikwa na 
  Emmanuel Makene

Wapendwa Wana wa Shinyanga;


UTANGULIZI
Kifo cha Mhashamu Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga, Mhashamu Aloysius Balina, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza siku ya Jumanne 06 Novemba 2012; kimeacha pengo kubwa kwa Kanisa Katoloki Tanzania
Askofu Balina amefariki akiwa amebakiza siku 10 tu afikishe miaka 15 kamili kama Askofu wa Jimbo la Shinyanga. Alikuwa ni Askofu wa tatu wa Jimbo la Shinyanga na wa kwanza wa Jimbo la Geita (Geita & Sengerema). Maaskofu wa Shinyanga waliomtangulia ni Askofu Edward Aloysius McGurkin aliyekuwa Askofu wa Shinyanga kati ya tarehe 04 Julai 1956 hadi alipostaafu 30 Januari 1975. 
Pia alitanguliwa katika kiti cha uaskofu wa Shinyanga na Askofu Castor Sekwa aliyekuwa Askofu wa Shinyanga kati ya tarehe 08 Agosti 1975 hadi O4 Juni 1996. Askofu McGurkin, ambaye alikuwa raia wa Marekani alifariki tarehe 28 Agosti 1983 na Askofu Sekwa alifariki tarehe 04 Juni 1996.
Kuna hadithi ambayo sikuwai kuidhibitisha; lakini inasemekana Askofu Balina alibatizwa kwa jina la ‘Aloysius’ baada ya wazazi wake kuchagua jina hilo ili afuate mifano mizuri ya kumcha mungu kama alivyofanya Padri Edward Aloysius McGurkin mbaye alikuwa Paroko wao. Na jambo hili kweli lilitimia kwani ‘Aloysius mkubwa’ na ‘Aloysius mdogo’ wote waliweza kuwa maaskofu kama nilivyoelezea hapo awali.
Askofu Balina alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya saratani ya ini kwa muda mrefu. Alikwishatibiwa Ujerumani na Vaticani, na akarejea nchini akiwa mwenye afya njema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...