Hivi ndivyo kura zilivyopigwa katika tukio hilo  lililojaa shamra shamra za aina yake na kuifanya Palestina kuibuka  kidedea na kupandishwa hadhi, kura 138 zilisema ndiyo, kula 9 zilisema hapana na kura 41 hazikufungamana na upande wowote. Tanzania kama ilivyokuwa kwa  nchi nyingine nyingi  ilipiga kura ya kuunga  mkono azimio hilo pamoja na kutoa sababu kwa nini imefikia  uamuzi huo. Ingawa  azimio hilo linaipandisha hadhi Palestina  na kuifungulia milango ya  kujiunga na taasisi nyingine za kimataifa, kama ikitaka kufanya hivyo,  bado inasafari  ndefu ya kufikia hatua ya kuwa mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa,  kutoka na kwamba ni lazima mchakato huo uanzie Baraza  Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa,  ambako Marekani imeleza bayana kwamba itapiga kura ya veto dhidi ya  ombi hilo
Rais wa Mamlaka ya  Palestina Mahmoud Abbas akilihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,  muda mfupi kabla ya upigaji kura wa Azimio la kuipandisha Hadhi Palestina kuwa  kama nchi muangalizi asiye mwanachama wa Umoja wa Mataifa,  tukio hilo la kihistoria limefanyika siku ya  Alhamisi hapa Makao Makuu ya  Umoja wa Mataifa.  
Habari kamili BOFYA HAPA


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. vipi azimio la kura ya Zanzibar huru litapigwa lini,tumechoka kukaliwaaaa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...