Wajumbe wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, wakipiga kura kupitisha Azimio la kuongeza muda wa vikwazo vya silaha na vikwazo vinginevyo kwa makundi ya waasi yanayoendelea kuleta vurugu na machafuko katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Mojawapo ya kundi la waasi linalobanwa na Azimio hilo ni lile la M23 ambalo hivi karibuni limetwaa mji wa Goma. Muda huo wa vikwanzo umeongezwa hadi februari Mosi 2014. Baraza hilo pia limesisitiza kwamba, mtu yoyote au taasisi inayojihusisha na kulisaidia kundi hilo la M23 kuacha mara moja la sivyo nao watakabiliwa na vikwazo vikiwamo vya kutosafiri na kusitishwa kwa mali zao.
Na
Mwandishi Maalum
Baraza
Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa , limepitisha kwa kauli moja azimio linaloongeza
muda wa vikwazo vya silaha na vikwazo vingine dhidi
ya vikundi vya waasi ambavyo viko katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)
Azimio
hilo nambari 2078 ( 2012) linaelezea pia
haja ya kuongeza vikwazo vya ziada kwa
uongozi na wapiganaji wa kundi la waasi la M23, kundi ambalo hivi
karibuni lilichukua Jimbo la Goma.
Baraza Kuu la
Usalama ambalo lilikutana siku ya
Jumatano limeongeza muda huo wa vikwazo hadi Februari Mosi mwaka 2014.
Vikwazo dhidi ya
silaha viliwekwa kwa mara ya kwanza mwaka 2003 mara baada ya kumalizika kwa vita vya
mara kwa mara nchini DRC, vita ambavyo
vimedumu kwa miaka mitano na kukadiriwa kuua zaidi ya
watu milioni tano.
Vikwazo vya silaha vimekwa dhidi ya makundi yenye silaha na ambayo si sehemu ya Jeshi la pamoja la Serikali au Polisi na pia vinahusu vikwazo ya kusafiri na
usitishwaji wa mali za watu au taasisi
ambazo zinakiuka vikwazo hivyo.
Azimio hilo pia linalaani vikali kundi la waasi la
M23, kundi ambalo linahusisha wanajeshi
walioasi kutoka jeshi la kitaifa la DRC mwezi wa Aprili mwaka huu. Kundi ambalo kwa sasa linashikilia Goma, ambao
ni Mji Mkuu wa
Kivu ya Magharibi.
Baraza Kuu linalitaka kundi hilo la M23 na makundi
mengine, kuacha mara moja aina zote za
mapigano au vitendo vinavyosababisha uvunjifu wa amani.
Aidha Baraza kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa
limeagiza na kurudia tena
kusitishwa mara moja kwa misaada
ya aina yoyote kutoka nje inayoelekezwa kwa kundi la M23.
Kama hiyo haitoshi,
Baraza Kuu la Usalama limeelezea
nia yake ya kupanua wigo wa vikwazo siyo
tu kwa viongozi wa M23 bali pia kwa
yeyote yule ambayo kwa namna moja ama nyingine analisaidia kundi hilo la M23 au
anakiuka vikwazo.
Wakati huo huo, Baraza Kuu la usalama pia limemwomba Katibu Mkuu wa
Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, kuliongezea muda
Kikundi cha Wataalamu
kuhusu DRC, hadi February Mosi
mwaka 2014 ili kiweze kufuatilia
utekelezaji wa vikwazo hivyo.
Katika hatua nyingine, Umoja wa Mataifa, umemtuma Mshauri wake Mkuu kuhusu
masuala ya Kijeshi, Jeneral Babacar Gaye
kwenda katika nchi za Maziwa Makuu ambako atakutana na kufanya majadiliano na
wadau mbalimbali kuhusu masuala kadhaa yaliyojiri hivi karibu wakati wa mkutano wa Viongozi wa Nchi za Maziwa Makuu ( ICGLR).
Masuala hayo ni
pamoja na utekelezaji wa kilomita 20
za Ukanda Huru ( Neutral Zone )eneo ambalo
M23 litatakiwa kuondoka, na dhana ya kuwa na Jeshi la Kimataifa lisilofungamana na upande wowote.
( International Neutral Force).



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...