SERIKALI inasikitika kutangaza kifo cha Bw. Jackson Makwetta kilichotokea Jumamosi saa 11 jioni katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ya jijini Dar es Salaam ambako alikuwa amelazwa.
 
Msiba uko nyumbani kwake Boko kwa Wagogo. Taarifa zaidi kuhusu mipango ya mazishi zitatolewa baadaye.
 
Bw. Makweta aliwahi kuwa Waziri katika wizara mbalimbali zikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu kama Waziri wa Nchi, Elimu, Kilimo na Utumishi.
 
Pia amekuwa Mbunge kwa zaidi ya miaka 35.
 
 IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
                                                      DODOMA.
                                                                   JUMAMOSI, NOVEMBA 17, 2012.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mungu amlaze pema peponi na amsamehe kwa yote.
    Nakumbuka mwaka nilioanza kidato cha kwanza tambaza akiwa waziri wa elimu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...