mmoja wa watoto akiwa amembeba mtoto mwenzake akiomba kupewa chochote kitu kutoka kwa wasamaria wema,kama alivyonaswa na Kamera ya Yetu,eneo la Fire,Morogoro Road jijini Dar.
Pichani juu ni watoto wakiomba omba chochote kitu eneo la Fire,Morogoro road,watoto hao wamekuwa wakiongezeka kila kukicha,nadhani imefika wakati pamoja na kwamba ni watoto wetu na si watoto wa mitaani kama baadhi ya watu walivyozoea kuwaita,Serikali inapaswa kuingilia kati na kuchukua hatua za dhati kabisa,kuinusuru hii hali na kuhakikisha Watoto wetu hawa hawaharibiki wangali wadogo kama waonekanavyo.
Pichani ni baadhi ya wazazi wenye watoto hao wakiwa wamejipumzisha kimyaa huku watoto wao ndiyo wakifanya kazi ya kuomba omba huku na kule ili wapate chochote kitu maisha yaendelee.Kiukweli watoto hawa wanapaswa kuhangaikiwa mapema sana kwa maana wana haki ya kulindwa na kuishi kwa amani na upendo kama wengine,Tusipokuwa makini tutajenga Taifa lenye matatizo makubwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Akina haki za binadamu wako wapi? Wepesi kuishtaki serikali mbona hawaingilii haya? Au haina maslahi kwao?

    ReplyDelete
  2. Haki ya Mungu tena wale waliokataa mimba na kutoroka waangalie vizuri watoto wao wako hapo!
    Mungu atuhurumie.
    Mimba zisozotarajiwa.
    Mimba zilizokatalia.
    Ubakaji.
    Umasikini
    na Ukosefu wa elimu (sina maana ya litabu hapa) Maana wako walisoma vitabu tu na wameacha watoto barabarani kama hivi! Mkitaka ushahidi mnitafute!
    Mungu ibariki Tanzania

    ReplyDelete
  3. In Conservation we say; don't feed the wild animals,because they will keep waiting for you to feed everyday,as a result they will not struggle to find food for themselves.
    The same applies to these human being, that's only because they are getting something everyday in this busness, then they will not stop doing it,the only solution is to give them nothing, then if they will face such a situation twice,thrice, or more, consequently they will stop wasting their time.
    But so long you give them something, they will not stop waiting for you to give.

    ReplyDelete
  4. Mabilioni ya pesa wanakula NGOs kila mwaka kwa mgongo wa hawa watoto!

    ReplyDelete
  5. siyo SWALA bali ni suala.

    Hili jambo la watoto kutangatanga na kuomba kwa kweli linasikitisha.

    ReplyDelete
  6. we anon uliyeandika kwa kiingereza kweli hamnazo...kwani hao watoto unafikiri watafanya kazi gani hapo mjini? ungeongea kuhusu NGO's na wazazi wao kufanya kazi zao ningekuona wa maana lakini kufananisha hao watoto na tabia za wanyama nadhani wewe ndo kama mnyama. usije ukashangaa na wako pia yuko humo. Le Profeseri nini?

    ReplyDelete
  7. Inasikitisha Serekali isiyojali watu wake..kuna jamaa alitaka kuchukuwa mtoto akamlee Belgium yeye na mkewake lakini mibongo namna ilivo na choyo ilimkatalia pamoja na kuhonga lakini wapi,wanajuwa mtoto akilelewa europ atafanikiwa kielimu and so on!!!wanafurahi kuona hivi...

    ReplyDelete
  8. Hivi usiku huwa wanalala wapi?bora hata hivyo vidume,lakini hivi vya kike ndivyo viko kwenye hatari zaidi.Miaka 12 tu watu wanaingia.

    ReplyDelete
  9. We Anony, unaemsema huyu aliye andika kwa kiingereza, hivi wewe huwaoni hao mama zao wanapiga story hapo nyuma ya magofu wanasubiri watoto warisk maisha yao kwa kukwepa magari,kwanini hao akina mama zao wasi shughulike hiyokazi ya kuombaomba,kuanza tu kumsema mwenzio bila kuangalia vizuri michuzi anasema nini siyo vizuri.

    ReplyDelete
  10. Kazi ya kutimiza jukumu hili ni ndogo sana!

    Ni kumkamata Fisadi mmoja kumfilisi halafu pesa yote kuyoka kwake vinafunguliwa vituo vya malezi vya Jamii ili kuwalea.

    Sio jukumu la kungoja Wahisani wenye Mashariti magumu kama Uingereza, UN WORLD BANK na IMF.

    Ni kupitia ufisilisi huo wa Mafisadi na jitihada zetu binafsi wananchi wa kawaida kuchangia malezi hayo.

    ReplyDelete
  11. Tatizo kubwa ni kuwa tunajua uzazi lakini malezi ahhh jukumu la wengine!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...