Wapenzi wa BBC, ndugu, jamaa na marafiki, 
 
Tunawaarifu kuwa ibada ya kumuaga ndugu yetu mpendwa Fred Mtoi, kwa walioko Uingereza itafanyika Jumamosi tarehe Mosi Disemba 2012 katika Kanisa la St. Anne's Lutheran mjini London kuanzia saa tano kamili asubuhi. 
 
Anwani ya Kanisa ni:
St Anne's Lutheran Church, 
Gresham Street, 
London
EC2V
 
Safari ya kuupeleka mwili wa marehemu Dar es salaam nchini Tanzania itakuwa Jumatatu tarehe 3 Disemba 2012 jioni kwa ndege ya Shirika la British Airways na kuwasili huko Jumanne saa moja asubuhi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere.
 
Shukran za dhati kwa Shirika la BBC kwa kushughulikia na kugharamia mipango yote ya kuusafirisha mwili wa marehemu Fred hadi Tanzania.
 
Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi kadri zinavyojitokeza kuhusu mipango ya msiba huu mpaka mwili utakaposafirishwa kwenda nyumbani Tanzania.
 
Idhaa ya Kiswahili ya BBC
 
Kwa maelezo zaidi wasiliana 
na Zawadi Machibya  +44 795 260 7038

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...