Wafanyabishara wadogo wadogo wanahitajika katika mahojiano ya utafiti (research interviews). Yafuatayo ni maelezo ya ziada juu ya msaada huu:
· Muhusika atakuwa anajishughulisha na kuwapigia simu washiriki (participants) na pia kupanga ratiba ya mahojiano.
· Kazi hii inaweza kufanyikia nyumbani.
· Itahusisha wahusika toka katika wilaya zote za mkoa wa Dar es Salaam (yaani; Ilala, Kinondoni, na Temeke).
· Mahojiano haya yanatarajiwa kuwa ya mwezi moja kuanzaia wiki lijalo.
· Malipo ni maelewano.
· Utafiti huu ni wa kiwango cha PhD.
· Washiriki ni wamiliki au maafisa wa biashara ndogo ndogo na za kati (owners of small and medium-size enterprises).
Sifa za muombaji
· Muombaji awe na elimu ya kidato cha nne au zaidi.
· Awe anaelewa maeneo mbalimbali ya jiji la DSM kwaajili ya kupanga mahali pa kufanyia mahojiano.
· Awe na uwezo wa kuandika na kuonge lugha ya kiingereza kama itahitajika.
· Awe na uwezo wa kufanya kazi bila ya kusimamiwa (being able to work independently).
· Awe na uwezo mkubwa wa kuwashawishi washiriki (convincing power).
Kama unaona unazo sifa na uwezo wa kazi hii,
basi wasiliana nami kwa kutumia email ifuatayo:
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...