Baraza
la Sanaa la Taifa limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za misiba ya
wasanii watatu wa tasnia ya filamu na muziki nchini.
“
Baraza limestushwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa ya vifo
hivi vya wasanii hawa John Mganga, Mlopelo na Hussein Mkeity a.k.a Sharo
Milionea ambao mchango wao unahitajika sana katika tasnia ya sanaa,
pengo waliloliacha ni kubwa kwani ubunifu wao bado unahitajika katika
tasnia hii.”
Baraza
linatoa pole kwa familia za marehemu na wasanii wote nchini, aidha
linawatakia moyo wa subira katika wakati huu wa majonzi ya kuondokewa na
wapendwa wetu.
Tunaomba
mwenyezi Mungu azipumzishe mahala pema peponi roho za marehemu. Baraza
liko pamoja na familia za marehemu katika kipindi hiki kigumu cha
maombolezo, tutambue kuwa haya ni mapenzi ya Mungu.
Imetolewa na
Ghonche materego
Katibu Mtendaji
Baraza la Sanaa la taifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...