Maofisa wa Benki
ya CRDB kutoka makao makuu Dar es salaam(Mkurugenzi wa wateja wa kati na
wadogo, meneja Mahusiano Tanzanite Akaunti,pamoja na Meneja wa biashara ya
kilimo) wako katika ziara ya kikazi nchini Oman kuanzia tarehe 18/12/2012 mpaka
29/12/2012.
Maofisa hao
wakiwa huko Oman watafanya mambo mengi yakiwemo;-
1.kukutana na wafanya biashara wa Oman wenye asili yakitanzania na
Watanzania kujadili fursa za uwekezaji na kujipatia mahitaji ya huduma za Benki
kwenye Biashara zao kupitia CRDB.
2.Kusimamia zoezi lakufungua akaunti za Tanzanite( Akaunti maalumu
kwa Watanzania walio nje ya nchi).
3.Pia watauza bidhaa nyingine za CRDB kama kupata huduma za kibenki
kupitia mtandao, kupata statement kwa njia a electroniki,Tembocard Visa na
Mastercard.
Siku ya Ijumaa tarehe 21/12/2012 watakua ofisi ya ubalozi wa
Tanzania nchini Oman kuanzia saa tatu asubuhi mpaka mchana kutoa huduma
zilizoainishwa hapo juu.
Siku ya Jumamosi tarehe 22/12/2012 watakuwepo katika mkutano na
watanzania utakaofanyika Crown Plaza Hotel Muscat kuanzia saa tatu asubuhi.
Kufungua akaunti utatakiwa kuwa na Picha 2, kopi ya hati ya
kusafiria pamoja na kianzio chenye thamani ya shilling 20,000 kwa TSH akaunti
au USD 50 kwa USD akaunti na fomu za
akaunti ya Tanzanite zilizosainiwa.
Kwamaelezo zaidi wasiliana na Meneja Mahusiano Tanzanite akaunti(Mr. Crispin M. Sichalwe) kwa namba ya
simu ifuatayo;+96899142025
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...