Shirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF) limepongeza bingwa mpya wa uzito wa Super Middle katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki yaa Kati, Mtanzania Francis Cheka, pichani juu.
Katika barua yake aliyomtumia Francis Cheka Mwenyekiti wa kamati ya Ubingwa wa IBF/USBA Lindsey Tucker alisema "Tunachukua fursa hii kukutakia maisha na mafanikio mazuri kama bingwa wa IBF na kumhimiza kuishi kama bingwa".
Cheka atatakiwa kutetea taji lake katika kipindi cha miezi sita kufikia mwezi wa 6 mwakani dhidi ya mpinzani ambaye ana rekodi ya mapambano yasiyopungua 15 na mengi awe ameyashinda hususan mapambano mawili ya mwisho.
Aidha IBF inampongeza bondia Chiotcha Chimwemwe kutoka Malawi kwa ushupavu wake na ushindani mzuri katika pambano hilo lililofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid katika jiji la Arusha tarehe 26 Desemba, 2012.
Imetolewa na:
Onesmo A.M. Ngowi
Rais
IBF/USBA Afrka, Ghuba ya Uajemi an Mashariki ya Kati
Du hii taarifa ya ushindi huu nilikua naisubiri kwa hamu maana hapa kaka cheka umeiwakilisha nchi kikwelikweli na amebeba hisia zote za wananchi ktk ushindi huu dhidi ya huyo mpinzani wako,nadiriki kusema mpinzani wako kaja ktk kipindi kibaya kwelikweli,Wa TZ wote tulikua tunabana nanihiii ili tuweze kufikisha ujumbe japo kwa njia ya ndondi, natumaini ushindi mwengine hauko mbali.Hongera cheka,hongera tanzania.
ReplyDelete