Wazalendo,
Napanda kuchukua nafasi hii kuwafahamisha kuwa kutokana na maombi ya
wanataaluma wengi kuwa mwishoni mwa mwezi desemba wanakuwa likizo.
Hivyo basi TPN imesikiliza maoni hayo na tumeamua kuisogeza mbele siku hii
ya wanataaluma Tanzania hadi mapema mwaka 2013.
Siku na Mahali tutawajulisha hapo baadae, mambo yote yaliyopangwa
yatafanyika.
Kutokana na kusogezwa mbele nachukua fursa hii kuwafahamisha kuwa bado
tunapokea maombi ya wanaotaka kutunikiwa tuzo; unaweza ukampendekeza mtu au
ukajipendekeza mwenyewe , ambatanisha CV na ueleze ni kwa nini upewe au
unayempendekeza apewe tuzo husika (soma email ya chin kwa maelezo zaidi).
Naomba tuendelee kushirikiana na kupeana ushauri kufanikisha siku hii.
Nawashukuru wote waliojitokeza kudhamini tukio hili na pia walijitokeza
kuchangia mawazo kufanikisha siku hii. Makampuni yaliyojitokeza kudhamini ni pamopja na ya umma na binafsi.
Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaosababishwa na kuahirishwa kwa tukio
hili ,naomba tuendelee kushirikiana.
Nawatakia wote kila heri ya kipindi hiki cha siku kuu za Krismasi,
mapumziko na Mwaka mpya mwema 2013.
Wanataaluma tuna nafasi ya kutumia taaluma zetu kuleta mabadiliko chanya kwa
faida ya Taifa letu.
Mungu awabariki wote,
Mungu ibariki Tanzania.
Phares Magesa
Rais- TPN
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...