Mkurugenzi wa Uendelezaji wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), David Shambwe akitangaza katika mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, muda wa kuanza kuuza nyumba 290 za bei nafuu zinazojengwa Kibada, Kigamboni,  zitakazoanza kuuzwa Januari 2, mwakani. Kulia ni Meneja Masoko na Utafiti wa NHC, Itandula Gambalagi. 
 Waandishi wa habari wakiwa kazini wakati wa mkutano huo uliofanyika leo NHC Kanda ya Kinondoni
 David Shambwe ( wa Pili kulia) akifafanua jambo katika mkutano huo. Kutoka kushoto ni Muungano Saguya ambaye ni Corporate Social Responsinbility Manager, Meneja wa Mkoa wa NHC Kanda ya Kinondoni, Erasto Chilambo na Meneja Masoko na Utafiti wa NHC, Itandula Gambalagi.
                                               Shambwe akiendelea kujibu maswali mbalimbali ya wanahabari

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. KAMA KUNA MTU ANAJUA BEI YA NYUMBA INA RANGE KIASI GANI ATUJULISHE

    ReplyDelete
  2. Masharti ya kununua/mnunuaji ni yapi? (Of Course ni lazima uwe na pesa, lakini kuna ni Mortgage au cash?)Na kama cash (I doubt)deposit ni kiasi gani? Au Mortgage, deposit ni kiasi gani? Taf toa maelezo kwenye blog kabla ya tar hiyo. Na wadau wa ughaibuni wakitaka kununua masharti ni nini na wao? Maana tunao ndugu zetu huho Ughaibuni wanataka kujua pia. Shukran.

    ReplyDelete
  3. hivi price ni siri!?,yani mkutano wote huo hakuna swala price nashindwa kuelewa

    ReplyDelete
  4. nashindwa kuelewa tuwekeeni bei mnaficha nini,

    ReplyDelete
  5. bei haitajwi hadharani, kwa wengi, "si bei nafuu" hata kidogo!bado tuna safari ndefu sana.

    ReplyDelete
  6. Vipi mbona ilikuwa rahisi kuwaita waandishi wa habari na kuweka kwenye mtandao tarehe ya kuuza nyumba hizo, inakuwaje vingumu kujibu maswali ya wadau kuhusu bei n.k. Haina haja kutueleza tarehe ya manunuzi wakati bei hatujui, eti 'bei nafuu" kiasi gani? Weka kwenye mtandao kabla ya siku

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...