Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi tuzo Mke wake Mama Salma Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA kwa kutambua mchango wa taasisi hiyo katika mapambano ya Ukimwi wakati wa maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani ambayo kitaifa iliadhimishwa mkoani Lindi kwenye uwanja wa Ilulu na kushirikisha wadau mbalimbali wanaopambana na janga la ugonjwa wa ukimwi nchini.Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Lindi,Mh. Ludovick Mwananzila.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi tuzo Meneja wa PSI Mtwara na Lindi kwa kutambua mchango wa taasisi hiyo katika mapambano ya ukimwi wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani yaliyofanyika jana mjini Lindi.Kushoto ni Mkurugenzi wa Tume ya kudhibiti Ukimwi TACAIDS Dr. Fatma Mrisho.
Mwenyekiti wa taasisi ya WAMA mama Salma Kikwete akifurahia tuzo hiyo pamoja na wafanyakazi wa taasisi yake mara baada ya kukabidhiwa na Rais Jakaya Kikwete jana katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika mjini Lindi
Wafanyakazi wa PSI wakionyesha tuzo yao mara baada ya kukabidhiwa kwenye maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani yaliyofanyika mjini Lindi jana.
Baadhi ya wafanyakazi na wadau mbalimbali walioshiriki katika maonyesho hayo kutoka WAMA.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia utiaji saini mkataba wa kusaidia Mpango wa kupiga vita ukimwi nchini Tanzania.Pichani Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu ndugu Peniel Lyimo,Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Ndugu Ramadhani Kija na Mkurugrnzi wa Global Fund Dr.Christopher Ben Wakitia saini Mkataba huo ambapo Global fund itatoa jumla ya Dola za Kimarekani milioni Mia tatu na nane (308 U S $) kwaajili ya Tanzania.Utiaji Saini Huo ulifanyika leo katika wanja wa michezo wa Ilulu yaliukofanyika maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani.Wengine wakishudia Utiaji saini mkataba huo ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete,Wziri wa Afya Dr.hussein Mwinyi na Bi Ursula Muller Mjumbe wa Bodi ya Global Fund 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiinua juu kitabu kuzindua rasmi mpango wa Kutokomeza maambukizi ya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto(Prevention From mother To Child Trsnsmission(PMTCT) wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani yaliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Ilulu mjini Lindi jana. Wengine katika picha ni mke wa Rais Mama Salma Kikwete(kulia),Waziri wa Afya Dkt.Hussein Mwinyi(wanne kushoto), Mkurugenzi wa Global fund Dkt.Christopher Ben(kushoto) na wapili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bwana Ludovic Mwananzila

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...