Rais Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akipokea ujumbe wa wasanii wakongwe wa muziki wa dansi pamoja na filamu kutoka kwa Kiongozi wa Wasanii hao,Waziri Ally (aliesimama) wakati ujumbe huo ulipomtembelea Ikulu jijini Dar es salaaam leo kwa kumshukuru Rais kwa kuwajali wasanii wa aina zote na hata kuamua kutoa tuzo kwa wasanii.ambapo mwaka huu amewatunuku Muhidin Maalim Gurumo na Hayati Marijani Rajabu.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akiwa katika mazungumzo na Kiongozi wa Band ya Kilimanjaro,Waziri Ally alieambatana na ujumbe wa wasanii wakongwe wa muziki wa dansi pamoja na filamu,Ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na ujumbe wa wasanii wakongwe wa muziki wa dansi pamoja na filamu uliomtembelea leo Ikulu jijini Dar es salaaam kwa kumshukuru kwa kuwajali wasanii wa aina zote na hata kuamua kutoa tuzo kwa wasanii.ambapo mwaka huu amewatunuku Muhidin Maalim Gurumo na Hayati Marijani Rajabu.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa wasanii wakongwe wa muziki wa dansi pamoja na filamu uliomtembelea leo Ikulu jijini Dar es salaaam kwa kumshukuru kwa kuwajali wasanii wa aina zote na hata kuamua kutoa tuzo kwa wasanii.ambapo mwaka huu amewatunuku Muhidin Maalim Gurumo na Hayati Marijani Rajabu.PICHA NA IKULU.
Serikali
imeanza kutoa Nishani kwa wasanii kwa vile inatambua umuhimu wao katika jamii.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete amewaeleza wawakilishi wa sanaa mbalimbali nchini
waliofika Ikulu leo asubuhi kutoa shukrani kwa Mheshimiwa Rais kwa kuwatambua
na kuwapa heshima kubwa ya Tuzo na Nishani wasanii katika siku ya sherehe za
Uhuru za tarehe 9 Disemba, Ikulu, Dar-Es-Salaam.
“Tumetoa
Nishani kwa vile wasanii wanatoa mchango mkubwa, tumeanza kutoa nishani mwaka
huu na tutaendelea kutoa miaka ijayo kwani kwa kuitambua sanaa, mnawapa moyo
wasanii kuendelea kujituma na kuwa wabunifu zaidi”
Rais amesema na kuongeza, “Tumeingiza Nishani ya Wasanii na Watafiti
maana nao wanafanya kazi kubwa sana ya kutafiti mazao na mbegu mbalimbali
ambazo zinaongeza tija katika kilimo nchini”.
Katika
kumbukumbu ya kusherehekea miaka 51 ya Uhuru
wa Tanzania bara mwaka huu, Rais Kikwete alitunuku nishani kwa makundi
mbalimbali ya watu waliotoa mchango mkubwa katika jamii na waliotumikia taifa
kwa uadilifu.
Rais
alitoa Nishani ya Sanaa na Michezo kwa mara ya kwanza kwa wasanii nchini ambapo
Bi. Fatma Baraka Khamis (Bi Kidude) kupitia Baraza la Sanaa Zanzibar, Kiongozi
wa Muziki wa Dansi ya Msondo Ngoma Muhidin Gurumo, Kiongozi wa Zamani wa Bendi
ya Dar Intrenational Marehemu Marijan Rajab walipata tuzo hiyo.
Wengine
ni Msanii wa maigizo na filamu nchini Marehemu Fundi Said (Mzee Kipara) na
Mwanariadha mkongwe John Steven Akwari.
Rais
amewataka wasanii kushirikiana na serikali lakini pia wawe mstari wa mbele
katika kupigania haki zao na sio kusubiri serikali tu iwafanyie hivyo.
Wasanii
hao wamefika Ikulu wakiongozwa na Bw. Ruge Mutahaba wa Clouds Media Group.
Wengine
ni Addo Mwasongwe, Rais wa Shirikisho la Muziki na Mwenyekiti wa Chama cha
Muziki wa Injili, Bw. Juma Ubao Mwenyekiti wa Chama cha Muziki Tanzania
(CHAMUDATA).
Bibi Shakila Said, Mkongwe wa Muziki wa Taarab
Nchini, Bi Carola Kinasha Msanii wa Muziki , Mzee King Kiki msanii wa Muziki wa
Dansi Mwana FA, msanii wa Kizazi Kipya na Bw. Waziri Ally , msanii wa Muziki.
Wawakilishi
hao pia wamemshukuru Rais kwa msaada wa hali na mali anaotoa kwa wasanii
mbalimbali wanapopata matatizo ambao hivi sasa wapo katika hatua mbalimbali za
matibabu ya afya zao hapa nchini na nchi za Nje.
“Haya
mengine ninayafanya tukama wajibu wa
kibinadamu kwa vile nina nafasi ya kufanya hivyo na pale tunapokua na
uwezo tunasaidia kama binadamu wenzetu”
Rais Amesema.
Imetolewa
na Premi Kibanga,
Mwandishi
Habari wa Rais, Msaidizi,
Ikulu
- DSM
21
Desemba, 2012
Hongera sana wasanii wetu kwa kwenda kumshukuru ndugu rais kwa mchango wake kwenu,ila na swali langu ni hili ktk picha namuona Ruge Mutahaba yeye alienda kama nani?! maana siyo mwanamumuziki naomba ufafanuzi wadau
ReplyDeleteAlienda kama mdau
ReplyDelete