Na Sixmund J. Begashe wa Makumbusho ya Taifa 
Tamasha kubwa la watoto la sanaa na Utamaduni linatarajiwa kufanyika Makumbusho na Nyumba Utamaduni kuanzaia tarehe 7 na 8 mwezi huu, ambapo vikundi zaidi ya 10 vya watoto chini ya miaka 15 vinatarajiwa kushiriki. Hayo yamwesemwa na Mkurugenzi wa Watoto Arts Organization (WAAO) Bibi Teresia Makene. 
Bibi Makene ameelaza kuwa hadi sasa vikundi vipo tayari na vimejiandaa vyema katika kulipamba Tamasha hilo la Watoto la Sanaa na Utamaduni, aliongeza kuwa Tamasha hilo litapambwa na Ngoma, Musiki, sarakasi, ngojera, Mashahiri, Sanaa za Ufundi na Sanaa shirikishi. 
Akielezea madhumini ya Tamasha hilo, Bibi Makene alisema kuwa Tamasha hili litawasaidia watoto kukuza vipaji vyao katika tasnia ya sanaa na Utamaduni, kuimarika kimaadili yenye kuzingatia mila na desturi za mtanzania, kuwajengea watoto tabia ya Uzalendo na kuutambua Uridhi wao kwa kupitia Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni. 
Bibi Makene ametoa wito kwa wazazi wa watoto kuwa wawalete watoto wao kwa wingi katika Tamasha hili la watoto, na pia Bibi Makene anaendea kutoa wito kwa wadau mbali mbali kujitokeza na kulisaidia Tamasha hili kwani linamanufaa makubwa kwa Taifa letu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...