Bondia Mtanzania Thomas Mashali kushoto akiwa amemgalagaza bondia Bernad Mackoliech na kwenda chini akimsubili ili amwendelezee kipondo wakati wa mchezo wao wa kugombania ubingwa wa Afrika Mashariki uliofanyika katika ukumbi wa Friends Conner, Manzese jijini Dar es Salaam na Mashali kuibuka na ushindi wa K,O katika raundi ya sita
 Bondia Bernad Mackoliech wa kenya na Mtanzania Thomas Mashali wakioneshana ufundi wa kutupiana makonde wakati wa mchezo wao wa ubingwa wa Afrika Mashariki Mashali alishinda kwa K,O raundi ya sita
Baadhi ya mashabiki waliojitokeza katika mpambano huo wa ubingwa wa Afrika Mashariki
Refarii Mark Hatia akimwesabia Bondia Bernad Mackoliech huku akimuamulu Thomas Mashalikwenda katika kona nyeupe baada ya kumtwanga konde zito lililomsababisha kulamba sakafu wakati wa mpambano wao wa ubingwa wa Afrika Mashariki 
Kamanda wa polisi mkoa wa Kipolisi wa kinondoni Charles Kenyela akimvisha ubingwa wa Afrika Mashariki bondia Thomas Mashali baada ya kumpiga Bernad Mackoliech wa Kenya kwa K,O Raundi ya 6.
Refarii Mark Hatia akimwesabia Bondia Bernad Mackoliech huku akimuamuru Thomas Mashalikwenda katika kona nyeupe baada ya kumtwanga konde zito lililomsababisha kulamba sakafu wakati wa mpambano wao wa ubingwa wa Afrika Mashariki picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. ALIVYOMGARAGAZA sio ALIVYOMGALAGAZA!!

    ReplyDelete
  2. "Piga ua galagaza" mi ntasema "ALIVYOMGALAGAZA".

    ReplyDelete
  3. Mie ntasema hongera bondia wetu kwa kuweka heshima ya nchi.Nafurahi zaidi kuona tasnia ya ngumi inavyofanya vizuri ktk ukanda wa afrika, tunajivunia mabondia wetu kwa sifa sahihi waileteayo nchi.Hongera Thomas Mashali kwa ushindi mzuri.

    ReplyDelete
  4. Piga ngumi Mkenya huyo!

    Akitoka hapo akavue Glovu na kuwahi Kericho akavune chai kwao Kenya mashambani!

    ReplyDelete
  5. Hatuwezi Wa Tanzania kukosa kila kitu!

    Mpira hatuna chetu, Riadha ndio kabisaaa na ngumi pia ?

    Haiwezekani ikiwa ngo'mbe hakupewa ndevu kama mbuzi basi ng'ombe atapata hata angalau sharubu tuu!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...