Habari Michuzi Team,
Naomba muipost hiyo picha hii ili wahusika waweze kufyeka hivyo vichaka. Hili ni eneo la njia panda ya chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM) karibu na daraja la Ubungo barabara ya Sam Nujoma. 

 Unapotoka Mlimani City ukifika njia panda hiyo kwenye mataa karibu na daraja, unapokata kwenda UDSM huwezi kuona vizuri magari yatokayo Ubungo mataa na hivyo ni rahisi kutokea ajali na hasa ukizingatia kuwa magari mengi huja kwa kasi eneo hilo. 

Naomba wahusika mlifanyie kazi swala hili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Asante sana mkuu kwa kukiona hicho kichaka kamkitu hatari sana kwa usalama.Hiyo watu wa usalama na Afya(safety and health) wanaita HAZARD(Hatarisho??).Yaani umegundua HAZARD.Sehemu zingine za kazi(zinazojali usalama wa wafanyakazi wake) ukigundua kitu kama hiki unaweza kupata zawadi.

    David V

    ReplyDelete
  2. Eh, usichokijua nini wewe.? Kila siku tunalalamika uharibifu wa misitu wewe unalalamika!

    ReplyDelete
  3. Kutokana na mvua zilizonyesha kwa mfurulizo, mahani yameweza kuota ghafla kuliko kawaida. Tunaahidi kusafisha hayo maeneo ndani ya siku mbili.

    ReplyDelete
  4. Umeongea vizuri, halafu unachanganya na maneno ya utani au? barabara na road kunatofauti gani? Tunapoelimishana ama kukumbushana kuwe na lugha inayoeleweka.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...