Mwenyekiti wa Mkutano Kujajidili Changamoto za Muungano,Mh. Mohamed Aboud Mohamed ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar akijadiliana jambo na Mwenyekiti Mwenza,Mh. Samia Suluhu Hassan ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano wakati kwa mkutano huo.
Baadhi ya Mawaziri wakiwa katika mkutano wa kujadili Changamoto za Muungano mjini Zanzibar leo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-Fedha,Uchumi na Maendeleo Zanzibar,Mh. Omary Yusuph Mzee (kushoto) akizungumza na Waziri wa Fedha na Uchumi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. William Mgimwa wakati wa mkutano huo.Picha na Ali Meja, Habari na Evelyn Mkokoi wa OMR.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa serikali ya mapinduzi Zanzibar mh. Mohamed Aboud Mohamed, ameongoza kikao cha mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kilichojadili masuala ya muungano huko Zanzibar leo.

Mambo mbali mbali yamejadiliwa katika kikao hicho, ikiwa ni pamoja na kupitia na kuthibitisha kumbukumbu za kikao cha Mawaziri kilichopita kilichofanyika mjini Dar es Salaam mwezi march mwka 2011, kupitia kumbu kumbu za kikao cha kamati ya pamoja ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Seriklai ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Mh. Aboud kama mwenyikiti wa kikao hicho cha mawaziri pia ameongoza mawaziri hao katika kupitia rasimu ya mwongozo wa ushiriki wa serilaki ya mapinduzi Zanziar katika masuala ya kimatifa katika hatua za awali.

Pamoja na hayo mambo mengine yaliyojadiliwa ni pamoja na,kupokea mapendekezo kuhusu uratibu wa muda wa mgao wa ajira kwa taasisi za muungano kwa serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania na serikali ya mapinduzi ya Zanzibar na kupitia taarifa ya utekelezaji wa masuala ya muungano.

Aidha kikao hicho pia kimeweza kupitia hati za makubaliano ya hoja zilizopatiwa ufumbuzi, na agenda za kikao cha kamati ya pamoja ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na serikali ya mapinduzi ya Zanzibar .

Mwenyikiti Mh. Aboud ameongoza kikao hiki cha mawaziri kwa kushirikiana na mwenyekiti mwenza  ambae ni waziri wa nchi ofisi ya Makamu wa Rais muungano  Mhe. Samia Hassan Suluhu ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kikao cha kamati ya pamoja kati ya serikali ya jamhuri ya muungano wa tanzania na serikali ya mapinduzi Zanzibar kitakachofanyika kesho mjini zanzibar chini ya uwenyekiti wa  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mh Dkt Gharib Mohamed Bilal.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...