Abiria wakiwa kwenye foleni ya kuboard kwa ajili ya safari ya kwenda sehemu mbali mbali duniani hivi sasa ,ndani ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,wakiwa na vitambaa vyao vya kufutia jasho huku wengine wakionekana kulowa jasho kwenye mashati yao baada ya kiyoyozi cha uwanjani hapo kutofanya kazi na haijulikani ni kwanini. sasa pata picha hapa ndani jinsi palivyo halafu watu wapo kwenye foleni namna hii na kiyoyozi ndio hivyo kimegoma,unafikiri inakuwaje??

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 21 mpaka sasa

  1. Hapo ni kwamba wanaingia ndani ya ndege wakiwa wameloa jasho na harufu itakuwa ni safari nzima hadi watakapooga na kubadili nguo. Bahati mbaya pia hakuna sehemu ya kuogea kama ilivyo ktk airport nyingine !!!

    ReplyDelete
  2. Inatia aibu kwa kweli. The first and last impression made by a tourist about a country is the point of entry and exit. This airport is beyond embarrassing for us Tanzanians, but of course the Ministry responsible is so clue less because they go through the VIP lounge. This situation can be a real deal breaker when after having had a wonderful holiday in and around TZ, this becomes your last memory of the country. Shame!

    ReplyDelete
  3. Kiyoyozi cha nini na hospitali vitanda havitoshi hata wagonjwa wanalala chini!!

    ReplyDelete
  4. Ally malaptopJanuary 17, 2013

    Dah umenikumbusha mbali wakati naingia bongo kutokea ng'ambo mara umeme umekata ikabidi milango ya kupitishia mizigo toka uwanjani iachwe wazi na mizigo yote jamaa wakaibeba na kuipanga mstari badala ya kuisubiri kwenye ile cheni lipite ulichukue

    ReplyDelete
  5. fezeha bin aibu iliyotukuka nchi inapata misaada wa mabilioni kila siku wanaweka saini za kupokea mabilioni

    uwanja wa ndege ambao ndio sura ya taifa maana kila mgeni akija kutoka nje ya nchi ni lazima ashukie hapo leo hii hali ni mbovu kuliko maelezo sehemu nyingine zinavujisha maji

    upo wapi mkuu mheshimiwa wa taifa piga chini watumishi wako wabovu wanakutia aibu kubwa na aibu kwa taifa lako

    ReplyDelete
  6. NA MIMI NIMEPITA HAPO HALI NI MBAYA NA INATIA AIBU. KINACHOTAKIWA KUFANYIKA NI KWAMBA TATIZO KAMA HILI LIKITOKEA WATU WA UHAMIAJI INABIDI WAONGEZE STAFF KWENYE MADIRISHA ILI WATU WAHUDUMIWE HARAKA. WATU WAKIPITA HARAKA USUMBUFU UTAPUNGUA. TATIZO LA JOTO LIKO HASA KENYE ARRIVAL HAPO WATU WALIPOPANGA FOLENI NA DEPARTURE. KWENYE KUSUBIRI MIZIGO WALAU KUNA HEWA KIDOGO...

    ps: na yule mwanaume wa public annoucement naye ajirekebishe kiingereza. Ana tatizo la 'TO' na 'IN'kila mara.
    ...anakazana 'Passengers proceed IN gate number....' angesema 'Passengers proceed TO gate number....'

    ReplyDelete
  7. Hapa Mwakyembe hajapatembelea, maana yeye hasafiri kwenda nje! Ngoja apate safari ya nje ndo atajua kero zetu kuhusu uwanja huu. Halafu tunalilia kumiliki ndege wakati AC inatushinda?

    ReplyDelete
  8. Hapo hatuna jinsi ila tu kuna mtu mmoja tu anayeweza kumaliza,tatizo sugu na ni Mhe,Mwakembe.au kwa lugha nyingine mwakembe ndiyo jibu,wizara husika.uwanja wetu ni mchafu sana pamoja na joto ni kero tupu.

    ReplyDelete
  9. kiyoyozi mbona ni kitambo kimekufa hapo ndo ujiulize hizo kodi za watanzania wanazolipa zinaenda wapi..yani ni upuuzi upuuzi tu

    ReplyDelete
  10. The money wasted to build a so called VIP terminal could have used to imprive the main terminal, tourist country who benefits the economy by bringing in much needed Forex used the main terminal which is in a such pathetic condition.

    ReplyDelete
  11. Kweli panatisha jamani duhhh!!!!!

    ReplyDelete
  12. ndo maana BA na airline nyingine zinaondoka
    aibu sana

    ReplyDelete
  13. halafu zinajengwa barabara za kupandia kati, mie huwa najiuliza wazee na walemavu watafikaje kati kupanda yale mabasi, lift umeme wenyewe huu, hivi serikali imewafikilia kweli wazee wetu na ndugu zetu wengine wasiojiweza jinsi ya kufika kati kupanda yale mabasi??????

    ReplyDelete
  14. Mwaka jana wakati nasubiri kumwona afisa uhamiaji kama hapo, nikakuta wabongo wanaruka mstari. Nikaenda mnbele yao na kuwaomba wasubiri kama wasafiri wengine. Walifikiri wakitumia maafisa wa uhamiaji kuruka mstari tutafunga midomo. Kwa bahati nzuri waliniheshimu na afisa mmoja mkubwa akawaambia wakae mstari kama wasafiri wengine. Mimi nilifoka sana mpaka wazungu nyuma nawasikia wakisema "jamaa atatiwa ndani sasa hivi". Inakera mno. kwanza hamna A/C halafu wabongo hawapendi kabisa kukaa mstari kama wachina kwao.

    ReplyDelete
  15. Give social services delivery to Private Operators and you'll see the difference!Ministry ihusike na masuala ya Security tu!tuache blah blah na kulalamika kwa sana,tupendekeze nini kifanyike hapao Airport kuboresha huduma za kijamii,na Waziri Mhusika,ayafanyie kazi mawazo na mapendekezo yetu!

    ReplyDelete
  16. Tanzania hiyo!!Apewe kagame watu wanyooke,viongozi wafikiria kuiba tu.no wonder watalii waishia Kenya tu

    ReplyDelete
  17. halafu mnangangania bandari bandari khaaa. wacha waondoke walishazoea kupuliza miperfume yao kwenye ndege eti sheria za kimataifa

    ReplyDelete


  18. Duh
    Kiwanja kinatishia amani,
    Rangi na matangazo huitaji mpangilio.
    Ila rangi na matangazo ya hapo yanonakana yanaashiria hatari

    ReplyDelete
  19. hapo tanganyika aibu tupu migration yapo slow kama nini uwanja mchafu hakuna hata kitu cha maana kinachoendelea hapo ni ujinga mtupu wapeni wazungu wawasaidie

    ReplyDelete
  20. Aibu sanaaa ukishuka airport ya bongo utadhani uko magereza panavyo nuka.......

    ReplyDelete
  21. Mtaishia kulalamika halafu mtatulia. Hawajali. Tanzania hiyo ndio ilivyo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...