
Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Paulina Mkonongo pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd sambamba na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya TDL wakiwa katika picha ya pamoja nje ya jengo la Wizara hiyo mapema leo,jijini dar

Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Paulina Mkonongo pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd ambao ni watengenezaji wa kinywaji cha Konyagi,David Mgwasa wakisalimiana na wanafunzi wanaosomeshwa na Kampuni hiyo chini ya Mpango wa kumuelimisha Mtoto wa Mkulima wa Zabibu unaojulikana kama ‘Zabibu na Shule kwanza’. Jumla ya wanafunzi 30 wanasomeshwa na Kiwanda cha Konyagi na wametembelea jijini Dar es Salaam kwa ziara ya kimafunzo.
Mmoja wa Wanafunzi,Chipengwa Yohana kutoka shule ya sekondari ya Handali,Dodoma Vijijini akiuliza swali kwa wafadhili wa mpango wa “Zabibu na shule kwanza”

Pichani kulia ni Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Paulina Mkonongo akifafanua jambo mbele ya Wahabari (hawapo pichani),kuhusiana na mpango wa kumuelimisha Mtoto wa Mkulima wa Zabibu unaojulikana kama ‘Zabibu na Shule kwanza’,shoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd ambao ni watengenezaji wa kinywaji cha Konyagi,David Mgwasa wanaoufadhili mpango huo.

Pichani kati ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd ambao ni watengenezaji wa kinywaji cha Konyagi,David Mgwasa akifafanua kwa kina mradi wanaoufadhili uitwao ‘Zabibu na Shule kwanza’ mbele ya anahabari jijini dar mapema leo,kulia kwake ni Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Paulina Mkonongo na shoto kwake ni Meneja masoko wa kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd,Joseph Chibehe ambao ni watengenezaji wa kinywaji cha Konyagi
====== ===== ======= =========
Mpango
huu wa kusomesha watoto wa mkulima unaojulikana kama “Zabibu na shule kwanza” ulizinduliwa rasmi mnamo tarehe 01 Julai
2011 Bungeni Dodoma na Spika wa bunge la Tanzania, mama Anna
Makinda.
Lengo
kuu la mradi huu ni kuhakikisha familia za wakulima walio kwenye mkataba na TDL
wanafaidia na kazi za wazazi wao kwa kusaidia watoto wa familia hizo kwenda
shule, kupunguza idadi kubwa ya watoto wanaoshindwa kuendelea na elimu ya
sekondari kutokana na kukosa pesa za kulipia ada na mahitaji muhimu ya
shule kutoka kwa wazazi ama walezi wao ambao ni wakulima wa zao la zabibu.
TDL
itakuwa imewapunguzia mzigo mkubwa na kuwapa wakulima hawa muda muafaka wa
kujitatiti zaidi katika shughuli za kilimo cha zabibu ili kuziwezesha
familia zao kujikimu vizuri kimaisha.
Mradi
huu ulianza na watoto kumi (10), na mwaka jana tukaongeza watoto ishirini (20) na
ni matarajio kuwa mwaka huu idadi ya watoto watakaopewa ufadhili itakuwa
wanafunzi ishirini (20), hivyo kufikisha idadi ya wanafunzi wanaosomeshwa na
mpango huu kuwa wanafunzi hamsini (50).
TDL
kama kampuni tunaamini kuwa, uwekezaji kwenye elimu na pia kumsomesha
mtoto ni kukuza uchumi wa nchi yetu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...