Na Mwandishi wetu

Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imewataka wasanii nchini kujitokeza kushiriki tamasha la sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki ambalo litafanyika nchini Rwanda mwezi ujao.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, kwa Niaba ya Katibu Mkuu, afisa Utamaduni Mwandamizi wa Wizara hiyo Makao makuu, Habibu Mohamed amesema tamasha hilo lijulikanalo kama JAMAFEST litafanyika kwa siku nane kuanzia Februari 9 hadi 16 mwaka huu.

“ Kwanza napenda kuwajulisha kuwa tumepata mwaliko wa kushiriki Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki, ‘JAMAFEST – 2013’ ambalo ni tamasha muhimu sana kwa wasanii wetu kushiriki katika hatua ya kutangaza na kuuza kazi zao katika soko la sanaa la Afrika Mashairiki,” amesema Habibu.

Amesema kutokana na mwaliko huo wa Jumuiya, Wizara inatoa mwaliko kwa wasanii, asasi, vikundi, wabunifu wa mavazi na kampuni kwa hapa nchini, ambao zitaweza kufanya maonesho na kuuza bidhaa na huduma za Sanaa na Utamaduni, katika mabanda ya Tanzania kutuma maombi yao wizarani ambapo mwisho wa kutuma maombi ni Januari 25.

Amesema washiriki watajigharamia nauli ya kwenda na kurudi, chakula na malazi katika kushiriki tamasha hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hivi kwenye barua za kikazi ukishaandika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuna haja gani ya kuandika chini yake United Republic of Tanzania??

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...