Hoyce Temu akimsikiliza kwa makini Rais wa serikali ya wanafunzi chuo cha Tumaini Iringa |
Hoyce Temu akipozi kwa picha na mzee wa matukio daima Francis Godwin baada ya kufanya mahojiano juu ya ziara yake mkoani Iringa |
Hoyce Temu alipojichanganya vidanda vya UVCCM na kukutana na wana ,mwanahabari wa Chanel Ten Clement Sanga , Afande Bashiri na mwanahabari Denis Mlowe |
Wadau wakifurahi kuwa na mrembo Hoyce Temu |
Miss Tanzania wa mwaka 1999 Hoyce Temu ametua mkoani Iringa na kujichanganya na wananchi wakazi wa mkoa wa Iringa katika maeneo ambayo si rahisi kwa star kama huyo kujichanganya .
Temu alishangaza wengi na kuonekana ni mtu wa watu baada ya kuacha kujirusha katika maeneo maarufu na kulazimika kujichanganya na wana Iringa katika Grosari za vibanda vya UVCCM mjini Iringa na kuwapa ofa ya kinywaji wadau waliofika kumsabai kwa salamu.
Hata hivyo Temu ambae yupo mkoani Iringa kwa ajili ya kuandaa kipindi chake cha MIMI NA TANZANIA kinachorushwa katika kituo cha Chanel Ten amesema kuwa lengo lake ni kuendelea kuheshimu taji lake kwa kufanya mambo mazuri katika jamii badala ya kujivunjia heshima yake .
Amesema kuwa atapenda kuona watanzania wanaendelea kumpongeza kwa kazi zake badala ya kuendelea kumdharau ,hivyo amesema ataendelea kufanya makubwa katika Taifa.
Kwa upande wake wakazi wa mkoa wa Iringa walimpongeza mrembo huyo kwa kazi nzuri anazozifanya katika jamii na kuwa katika maisha yake hapaswi kuiga mambo ya warembo wengine ambao wameshindwa kujiheshimu na kuonekana ni wachafu wa kutupwa katika jamii kutokana na kuwa na skendo kila kukicha.
Bila kuwataja majina ya warembo hao walisema kuwa picha ya kuwa urembo ni uhuni imekuwa ikichafuliwa na warembo wanaoshika nafasi kama hizo na mara baada ya kuwa maarufu wanaanza kuutumia umaarufu huo kuuza miili yao.
SAFI SANAA TEMU UNAFANYA MAMBO MAZURI SIO KUZEEKA NA MAMBO YA KITOTO.HIMO
ReplyDelete