Askari Polisi wakiwa wanashusha magunia ya bangi ambayo yalikuwa yanasafirishwa kutoka Arusha kuelekea Dar es salaam kwa gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T 282 AAJ
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi Liberatus Sabas akiwaonyesha waandishi wa habari madawa ya kulevya aina ya bangi ambayo yalikamatwa na jeshi hilo tarehe 07/02/2013. Picha na mahmoud ahmad wa Globu ya Jamii, Arusha


Na Rashid Nchimbi wa 
Jeshi la Polisi Arusha

Jeshi la Polisi mkoani hapa limemkamata mtu mmoja akiwa na magunia 97 ya madawa ya kulevya aina ya bangi ambayo yalikuwa yanasafirishwa toka mkoani hapa kuelekea Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi Liberatus Sabas amesema kwamba, tukio hilo lilitokea muda wa saa 10:00 alfajiri eneo la Usa River wilayani Arumeru.

Alisema mafanikio hayo yametokana na ushirikiano mzuri kati ya jeshi hilo na wananchi ambapo taarifa za tukio hilo zilitolewa na raia wema ambapo askari wa jeshi hilo waliweka mtego eneo hilo na kufanikiwa kulikamata gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T. 282 AAJ.

Kamanda Sabas aliongeza kwa kusema kwamba, ndani ya bodi ya gari hilo kulikuwa na mboga aina ya kabeji iliyosambazwa vizuri huku chini ya mboga hiyo kukiwa na madawa hayo yaliyokuwa kwenye magunia huku yakivingirishwa kwenye mifuko ya “plastiki” kwa ndani.

Alisema katika gari hilo kulikuwa na watu watatu na mara baada ya askari hao kulisimamisha dereva pamoja na msaidizi wake walifanikiwa kukimbia huku mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Praygod Marick (22) Mkazi wa Dar esalaam akikamatwa.

Jeshi la polisi Mkoani hapa linaendelea kumhoji mtuhumiwa huyo huku watuhumiwa wengine wakiendelea kutafutwa. Kwa mara nyingine tena Kamanda huyo aliendelea kuwashukuru wananchi wa Mkoa huu kutokana na ushirikiano wao mkubwa wanaoutoa kwa jeshi hilo na kuendelea kuwasisitizia kuimarisha mahusiano na jeshi hilo.

Kwa muda wa kipindi cha mwezi mmoja toka Januari 07, 2013 mpaka hivi leo jeshi hilo limeshakamata madawa ya kulevya aina ya mirungi magunia 372 katika magari mawili tofauti na pia limeshakamata jumla ya magunia 117 ya madawa ya kulevya aina ya bangi ambapo mwanzoni mwa wiki hii jumla ya magunia 20 yalikamatwa yakiwa yanasafirishwa kwa kutumia wanyama aina ya Punda maeneo ya Losoiti wilayani Longido.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Mkuu Sabas, unaposhika mihadarati ushikage huku ukiwa umevaa "Gloves"
    Ni ushauri tu

    ReplyDelete
  2. hivi jamani hizo biashara zimeanza leo huko arusha? mbona miezi hii tu ndio habari za kukamatwa kwa bangi zimeshika moto au kuna afande katoswa ulaji?

    hapo lazima itakuwa kuna afande kakosa ulaji sasa kaamua kuwatia adabu hao wauza bangi kwa kukamata mizigo yao yote

    bange ipo miaka nenda rudi sasa iweje ikamatwe hizi siku tu?

    haya hongereni sana maafande arofonso.

    ReplyDelete
  3. Mdau wa kwanza ukiona hivyo ni kuwa huyo Bosi aliyepita alikuwa anakula nao hao watu ndio maana mambo hayakuwa yanaharibika!

    Sasa nadhani huyu Bwana Mkubwa Kamanda aliyeingia sasa, kama sio Mlokole atakuwa ni Kijukuu cha Nyerere,,,watapita wapi?

    ReplyDelete
  4. Haaaa,!

    Magunia 97 si lori zima hilo?

    Inakuwa kama ni mzigo wa mahindi au mchele wa chakula vile?

    Ndio maana idadi ya machizi ni kubwa sasa nchini!

    ReplyDelete
  5. fereeeeee chezea arusha kwa bangi,

    ReplyDelete

  6. Nakubaliana mia kwa mia na ANON wa kwanza,

    KAMATENI MARUNDO KAMA HAYA YA COCAINE, HEROINE, SILAHA HARAMU, PASSPORT ZINAZOUZWA KWA WASIO RAIA, MAKONTENA YALIOJAA WAHABESHI HAPO TUTASEMA NDIO.

    SIO MARUNDO YA MAJANI ETI MADAWA YA KULEVYA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...