Na Freddy Macha
Maonyesho maarufu ya mavazi ya kimataifa –London Fashion Week- yatamega kitengo chake cha kimataifa kusaidia kutangaza kazi za washoni wapya toka Tanzania ndani ya Ubalozi wetu leo Ijumaa mjini London.
Mada ya maonyesho haya yatakayoendelea kwa juma zima  ni “Swahili Flavour” (Ladha ya Kiswahili). Yametayarishwa kwa ushirikiano wa Ubalozi wa Tanzania London na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kujenga vipaji na kazi za mavazi za washoni wasiofahamika duniani. 
 Kazi zitakazooyeshwa ni za washoni watatu Christine Mhando (anayetumia jina la ubunifu:  “Chichia London”),  Anna Lukindo ( “Anna Luks”) na Jacquleine Kibacha (“Heart 365”).
Mbunifu Christine Mhando
 Christine Mhando alihitimu chuo cha Usanii cha Kent mwaka 2002 na huhimiza mtindo wa Kanga na misemo na manen ya Kiswahili mathalan “Tongoza” na “Zungumza” kama wajihi wa kazi zake.  Anna Luks aliyesomea shahada yake chuo cha Middlesex, London hutumia vitambaa vya Kitanzania, kushona kwa mikono, kamba kamba, mavazi ya kike na dunia ya kisasa.  Baada ya kujiuzulu toka kazi ya kuajiriwa (kupanga sera)  Jaquileine Kibacha aliamua kufuata ndoto zake za kuwa msanii. Ubunifu wake unaochanganya desturi za kijadi na kisasa kutumia shanga shanga, manyoya ya ndege na mapambo imesanifiwa kutokana na safari aliyoifanya kuishi na Wamasai.
Kina  dada hawa  wanasisitiza kwamba  wana lengo la kukuuza sanaa na ubunifu, utamaduni wa Kitanzania, kutangaza taswira za Kiswahili na sura mbalimbali za Afrika Mashariki.
Kaimu Balozi wa Tanzania, Mheshimiwa Chabaka Kilumanga alisema kwamba maonyesho haya ya kimataifa yatakua nafasi kubwa kwa Tanzania kujenga jina  na ni sehemu mahsusi ya kujivunia utamadunina nchi  yetu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...