k6 Mchezaji wa timu ya waendesha Bodaboda kutoka Tegeta akiwania mpira mbele ya mchezaji wa timu ya Waendesha Bodaboda kutoka Kawe katika mashindano ya ligi ya Bodaboda Cup inayoendeshwa na Jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani ambapo timu ya Kawe imeifunga timu ya Tegeta kwa magoli 3-0 kwenye mchezo uliofanyika katika uwanja wa Tanganyika Pakers Kawe jijini Dar es salaam leo.

Mashindano hayo yanashirikisha timu za mkoa wa kipolisi wa Kinondoni ambazo zinatoka katika maeneo ya Kimara, Kawe, Tegeta, Mabibo na Ubungo wachezaji wakiwa ni waendesha Bodaboda, awamu ya kwanza ya ligi hiyo ilikuwa na timu 32 na sasa ni awamu ya pili ambapo timu 16 zinashindana ili kupata timu 8 zitakazoshiriki hatua ya Nane Bora na hatimaye kupata mshindi wa mashindano hayo ya Kinondoni Bodaboda Cup ambaye atapata zawadi nono.

Lengo la Mashindano hayo ni kuwakutanisha waendesha Bodaboda wote wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni ili waweze kufahamiana wao kwa wao, lakini pia ili jeshi la polisi Kikosi cha Usalama Barabarani liweze kuwaelimisha juu ya sheria za usalama Barabarani na Ulinzi Shirikishi kwa jamii.
k9 Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Agatha Isack akikagua timu kabla ya kuanza kwa michezo hiyo leo kwenye uwanja wa Tanganyika Pakers jijini Dar es salaam.
k10 Mkaguzi msaidizi wa Jeshi la polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Agatha Isack akikagua timu kabla ya kuanza kwa michezo hiyo leo kwenye uwanja wa Tanganyika Pakers jijini Dar es salaam.
k1 Timu ya Kawe ikiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa mchezo huo na kupata mawaidha mawili matatu.
k2 Kikosi cha timu ya Tegeta kikiwa katika picha ya pamoja kalba ya kuanza kwa mchezo huo timu hiyo imefungwa magoli 3-0 na timu ya Kawe.
k3 Baadhi ya mashaifuatilia mchezo huo.
k5Wachezaji wa timu za Kawe na Tegeta wakiwania mpira uliojuu wakati wa mchezouliokutanisha timu hizo leo kwenye uwanja wa Tanganyika PakersKawe jijini Dar es salaam
k8Kutoka kulia ni Aghata Isack Mkaguzi Msaidizi Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Esther Ngaja Mkaguzi Msaidizi Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Refarii wa mchezo huo Geofrey Mwamboneke, Mshika Kibendera Hamis Pondamali, Mshika Kibendera Mwanahamisi Matiku, ASP. Emilian Kamuhanda Insp.Soud Ramadhan na Mratibu wa kombe hilo Ernest Mbaga wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo uliofanyika kwenye uwanja wa Tanganyika Pakers leo,
k7 Mashabiki wakijikinga na jua huku wakifuatilia mchezo huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. MKAGUZI WA TIMU HII HEBU FANYA MAZOEZI UPUNGUZE MWILI, TUNATAKA WATU FIT YAAA.

    ReplyDelete
  2. Ndiyo maana mimi nimeacha kuvaa Suruwali.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...