Padri Evaristitus Mushi
Padri Evaristitus Mushi wa KANISA la Katoliki,Parokia ya ST.Joseph,Shangani,Unguja ameuwawa leo mnamo saa moja asubuhi katika eneo la Beit-el-Ras karibu na kanisa la Katoliki.
Kwa mujibu wa taarifa iliotolewa na Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Mhe. Mohamed Aboud imeeleza kuwa kutokana na tukio hilo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeliagiza Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina ili kuwatambua wale wote waliohusika na tukio hilo kwa ajili ya kuwachukulia hatua zinazofaa kwa mujibu wa sheria.
Mhe. Aboud amesema kuwa wakati uchunguzi huo unaendelra, Serikali inawaomba wananachi wote kuwa watulivu na kuliachia Jeshi hilo la Polisi kutekeleza wajibu wake.
Aidha Serikali imetoa mkono wa pole kwa familia na wanafamilia wa marehemu pamoja na waumini wa kanisa hilo kuwa wastahamilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
Padri Evaristitus Mushi wa KANISA la Katoliki,Parokia ya ST.Joseph,Shangani,Unguja ameuwawa leo mnamo saa moja asubuhi katika eneo la Beit-el-Ras karibu na kanisa la Katoliki.
Kwa mujibu wa taarifa iliotolewa na Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Mhe. Mohamed Aboud imeeleza kuwa kutokana na tukio hilo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeliagiza Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina ili kuwatambua wale wote waliohusika na tukio hilo kwa ajili ya kuwachukulia hatua zinazofaa kwa mujibu wa sheria.
Mhe. Aboud amesema kuwa wakati uchunguzi huo unaendelra, Serikali inawaomba wananachi wote kuwa watulivu na kuliachia Jeshi hilo la Polisi kutekeleza wajibu wake.
Aidha Serikali imetoa mkono wa pole kwa familia na wanafamilia wa marehemu pamoja na waumini wa kanisa hilo kuwa wastahamilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
Naomba kuuliza kwani nchi hii haina makachero? Serikali kila siku ni kuomba moyo ya subira na utulivu. Hao makachero wameajiriwa wanakula pesa za bure? Zanzibar ni nchi ndogo sana kweli hili lisijulikane kwa wiki hata wiki 4 basi???? hata kama si maswala ya ukristo na uislamu tuelezwe tusiachwe kigazani na kujenga mioyo ya chuki na hisia
ReplyDeleteR.I.P Mushi,
ReplyDeleteMungu tuepushe na haya majanga!
Serikali sasa inashindwa kazi. Haijifunzi kutokana na matukio yaliyotangulia kama yale ya yule Padri aliyepigwa risasi. Kila siku ni kuomba utulivu. Serikali lazima ielewe kuwa utulivu una mipaka yake pia. Watu watachoka kuwa watulivu mambo haya yakizidi kuendelea.
ReplyDeleteIt's quite devastating, heartbreaking and intolerable. How long will Christians be reminded of our values & moral duty to remain ' humble, submissive & persevering'? Our Holy teachings say it so clear. However, states & governments are in our belief, God given authority (ies). They have a duty to ensure all it's citizens irrespective of their differences, more so religion to,peacefully enjoy this basic right of WORSHIP & FAITH! We need action before things gets to worse from this bad scenario. We are all human beings with two sides of our being, the good & the bad. Let us respect each other! Neighbor principle should prevail.
ReplyDeleteMdau wa mwanzo suali lako kwa kiasi ni zuri lakini nadhani umeshau kuwa kila kukicha sio zanzibar tu bali tanzania nzima watu wanauliwa na serikali haifanyi lolote.
ReplyDeleteKifo hiki kimesikika tu kwa sababu ya wadhifa wake, lakini ndugu zetu tele wa albino kwa mfano wanauliwa kila leo na hata katika redio hairipotiwi seuze kwenye internet na kwengineko.
watu wanauliwa kila siku na serilai haitoi kauli yeyote ile, mifano ipo tele hapa zanzibar na wala sikusudii mauaji ya kidini au siasa ni mauaji ya wizi na ugomvi wa mitaani tu.
Wauaji wanasahau kwamba Jehanamu ya milele inawangoja kama hawatatubu.Mungu si mtu aseme uongo;Wala si mwanadamu,ajute;Iwapo amesema hatalitenda?Iwapo amenena, hatalifikiliza?Hizi ni nyakati za mwisho.Chukua hatua
ReplyDeleteJamari sasa too much!! Vita hii ipo wazi wazi Serikali isije kimya Lazima something must be done
ReplyDeleteHaya yote yasingetokea kama Watanzania tungeacha kushabikia udini!
ReplyDeleteKuna watu wanamchukia Rais tu kwasababu ya dini yake lkn.hakuna baya lililotokea ambalo ni kubwa na halijawahi kutokea hapa.
Watu na magazeti hawataki kumpa ushirikiano badala yake wanabaki kumlaumu na kumchafua lakini na sisi tunasema lazma amalize mda wake!..nchi ni yetu sote hii!