MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BANDARI TANZANIA
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inapenda kuwatangazia Wateja na Watumiaji wote wa Bandari kwamba imeanzisha Kitengo Maalum cha Huduma kwa Wateja kitakachopokea malalamiko, kero, taarifa, maoni, ushauri juu ya huduma mbalimbali zinazotolewa na Mamlaka.
Kuanzishwa kwa Kitengo hiki ni moja kati ya Mikakati ya Mamlaka ya kuboresha huduma zake na kuondoa kero kwa Wateja na Watumiaji wa Bandari.
Kwa huduma ya haraka tafadhali piga namba zifuatazo;
0754 292998
0756 849868
0788 888801
0789 334398
Namba hizi pia zinapatikana kwenye mtandao wa TPA www.tanzaniaports.com
MENEJIMENTI
Mnabidi mbadilike siyo msubori Mwakyembe awaongoze kila kitu . TAtizo lililopo Tanzania n kuwa watu wanafanya kazi kwa mazoea ili mradi pesa imeingia siku imepita basi . Hawana motivation ya kuongeza tija
ReplyDeleteHuduma kwa Wateja! Kitengo muhimu kisichotiliwa maanani na bahati mbaya hata walionacho wengine ni hovyo kabisa. Kwa mfano makampuni mengi ya simu ukipiga simu ya huduma kwa mteja sio wote wanaotoa huduma hiyo wanaelekea kujua "bidhaa muhimu za kampuni yao" Nenda kwenye benki za walalahoi, utakuta unataka kuuliza kitu tu wahusika wanakungalia kama uchafu! YEYOTE ANAEFANYA KAZI KWENYE KITENGO CHA AINA HII TAFADHALI BADILIKENI, WAPYA ZINGATIENI TAALUMA ZENU.
ReplyDeletesesophy
Mbona namba za Zantel, Tigo na TTCL hakuna??
ReplyDelete