Jaji Mkuu wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, Mhe. Mohamed Chande Othman akisaini kitabu cha wageni alipotembelea ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Mwanza asubuhi hii. Kushoto ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Tume, Mhe. Fakih Jundu. Mhe. Jaji Mkuu pamoja na ujumbe alioambatana nao wapo mkoani humo kwa ajili ya kuongea na wajumbe wa Kamati ya Maadili ya Mkoa huo lengo likiwa ni Kujenga mahusiano mazuri ya kiutendaji na Kamati Hilo. |
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, Bw.
Hussein Kattanga akiongea na wajumbe wa Kamati ya Maadili ya Mkoa wa Mwanza katika mkutano unaofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu mkoani
Mwanza hivi sasa. Mbali na kuwa Katibu wa Tume, Bw. Kattanga pia ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama
ya Tanzania.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Maadili ya mkoa wa Mwanza wakiwa Katika mkutano na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Picha na mdau Mary Gwera, Mahakama ya Tanzania
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...