Habari na picha na Dixon Busagaga,
Globu ya Jamii Moshi
WANARIADHA kutoka mkoa wa Arusha wamefanya vizuri katika mashindano ya
mbio za Taifa za Nyika zilizofanyika jana mjini Moshi kwa kupata
ushindi wa jumla baada ya wanariadha wake kushika nafasi za kwanza na
pili katika mbio za kiliometa 12 ,nane na sita .
Mashindano hayo ambayo awali yalikuwa yafanyike mkoani Morogoro
yaliowakutanisha wanariadha zaidi ya 100 kutoka mikoa mbalimbali
nchini na kufanyika katika viwanja vya klabu ya gofu ya mjini Moshi
baada ya kusimama kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita.
Katika mbio za utangulizi za kilomita 6 wanawake , Anjeline Irene
21:19;57, Selina Amosi 21:31:86, Fadhila Salum wote kutoka Arusha mbio
za km 8 wanawake Jaeldine Sakilu (JWTZ-Arusha) 27:00:34, Zakia Mrisho
(Arusha) 27:24:58 na Catherine Lange (Manyara) 28:12:91.
Katika upande wa wanaume km 8, Dotto Ikangaa 23:53:95 JWTZ-Arusha,
Joseph Theophil Mbulu 23:56:41 na Mohammed Ally 24:13:54 JWTZ- Arusha
huku mbio za km 12 wanaume akichukua Dickson Marwa 36:34:52 kutoka
Holili-Kilimanjaro.
Awali akizungumza na waandishi wa habari mapema kabla ya kuanza kwa
mbio hizo, Rais wa Shirikisho la Riadha Taifa, (RT), Anthony Mtaka
amesema kuwa madhumuni ya mbio hizo, ni kuandaa kikosi kitakacholiwakilisha Taifa katika mbio za Nyika za dunia zitakazofanyika Machi
24, nchini Poland pamoja na kuibua vipaji vya riadha nchini.
Mtaka amesema kuwa sababu za kuhamishia mbio hizo mkoani Kilimanjaro
ni kutokana na mdhamini waliyempta hapo awali kujiondoa na hivyo
kuwalazimisha kutafuta mdhamini mwengine ambapo alisema, Executive
Solution walisaidia sana.
Nao baadhi ya wanariadha walioshiriki mbio hizo, Jackline Juni,
aliyeshinda mbio za km 8 wanawake na Dickson Marwa, aliyeshinda mbio
za km 12 wanaume, walisema wako tayari kuiwakilisha nchi katika mbio
za Poland lakini walisisitiza umuhimu wa kuwepo kwa maandalizi na
ushirikiano kutoka kwa wadau wa Riadha.
Jumla ya wakimbiaji wapatao 100 kutoka katika mikoa ya Mwanza, Arusha,
Manyara, Singida, Mara, Zanzibar, mbeya, Dar es salaam na kilimanjaro
walichuana jana katika mbio za Nyika za taifa zilizofanyika katika
uwanja wa gofu wa Moshi Club ulioko katika Manispaa ya Moshi Mkoani
Kilimanjaro ambapo mshindi wa kwanza alipokea zawadi ya Sh. 60,0000.
Mwandishi wa habari wa shirika la utangaza TBC
Sauda Shimbo akifyatua bastola kuanzisha mbio za kiliometa 8 kwa
wananwake wakati wa mbio za nyika zilizo fanyika mjini Moshi .
Wanariadha wa mbio za kilometa 12 wakianza mbio
hizo .
Mwanariadha Banuelia Bryton Mrashani wa klabu ya
Holili mwenye nguo nyeusi akichuana na mwenzakeambaye jina lake
halikufahamika mara moja wakati wa mbio za nyika zilizofanyika mjini Moshi.
Rais wa shirikisho la riadha Tanzania ,Anthony
Mtaka (Shoto )akiteta jambo na mgeni rasmi wa mbio za Nyika za taifa
ambaye pia ni mkuu wa chuo cha polisi Moshi , Afande Matanga Mbushi.
Washiriki wa mbio za kilimeta 8 kwa upande wa wanawake
wakijiandaa ,kabla ya kuanza kwa mbio hizo za nyika
zilizofanyika katika viwanja vya Gofu mjini Moshi.
Rais wa shirikisho la soka Tanzania Anthon Mtaka
akizungumza na wanahabari wakati wa mbio za nyika zilizofanyika
mjini Moshi.
Mbio za nyika
Mshindi wa mbio za kilometa 12 kwa wavulana
Dixon Marwa wa klabu ya Holili akimaliza mbio hizo kwa nafasi ya kwanza
baada ya kutumia dakika 36 na sekunde 34 huku akimuacha mbali
mshindani wake Damiani Foka.
Huyu Mtaka ni wa Shirikisho la Soka au la Riadha? Maana naona katambulishwa mara mbili mbili kwa vyeo vyote viwili.
ReplyDelete