Na Anna Nkinda – Magu

Jamii imetakiwa kufanya kila iwezalo ili kuhakikisha kuwa watoto wa kike wanasoma na kupata elimu bora kwa kufanya hivyo kutawasaidia watoto hao kuweza kupambana na changamoto mbalimbali zinazowakabili katika maisha yao.

Wito huo umetolewa hivi karibuni na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati akiweka jiwe la msingi la jengo la Hosteli ya wasichana ya chuo cha sanaa na ufundi Bujora kilichopo wilayani Magu katika mkoa wa Mwanza.

Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alisema kuwa ni wajibu wa jamii kuwatengenezea watoto mazingira mazuri ya kusoma ikiwa ni pamoja na kuwajengea Hosteli ambayo itawasaidia kuishi shuleni na hivyo kuepukana na vishawishi ambavyo vinaweza kuwahatarishia masomo yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...