Kituo cha mafuta cha Oil Com kilichopo eneo Nane Nane mjini Morogoro kimekamatwa leo kwa wizi wa umeme baada ya kuharibu mita ya umeme kwa kuweka rezista kwa lengo la kupunguza upimaji wa mita ya umeme. Kituo hiki ni cha pili kukamtwa na kikosi cha ukaguzi toka makao makuu, ndani ya masaa mawili yaliyopita na kituo kingine ni cha Oil Com kilichopo eneo Kihonda
 Mafundi wa Tanesco wakitoa waya zote za umeme zilizokuwa zinapeleka umeme Oil Com baada ya kukamatwa kwa wizi wa umeme
 Kituo cha mafuta cha Oil Com kilichopo katika eneo  Kihonda Mkoani Morogoro kimekamatwa kwa wizi wa umeme na kikosi cha ukaguzi toka makao. Ni hujuma na ambazo kama zikiendelea ni hatari kwa uhai wa Shirika hili la umma.
 Meneja wa Kituo (kushoto) akipewa maelekezo baada ya kushuhudia mita ilivyoharibiwa
 Mita ya umeme iliyoharibiwa toka Kituo cha mafuta cha Oil Com kilichopo eneo Nane Nane.
 Mita iliyoharibiwa kwa kuwekewa rezista kupunguza upimaji wa mita
Meneja wa kituo cha mafuta cha Oil Com kilichopo eneo Nane Nane ambaye ndiye meneja wa kituo cha mafuta cha Oil Com kilichopo eneo la Kihonda (kulia)akishuhudia mita ya umeme iliyoharibiwa ikijaribiwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...