MREMBO Mary Rutta kutoka Mkoa wa Manyara jana usiku aliwabwaga warembo wenzake 26 katika kinyang’anyiro cha kumsaka mrembo wa Miss Utalii mwenye kipaji. Kinyang’anyiro hicho kilifanyika Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live.
Mary Chrisostom Rutta, kutoka Mkoa wa Manyara (katikati) akifurahi baada ya kutangazwa mshindi. Kushoto ni Jamia Abdul (Kagera) na Joan John kutoka Lindi ambao waliingia tatu bora.
Mary na warembo wenzake wakishangilia ushindi huo.
Warembo wakionesha vipaji kwa kucheza ngoma za asili.
Wakionesha vazi la ubunifu.
Msanii wa ngoma za asili kutoka Bagamoyo, Chemundu Gwao, akicheza na warembo hao.
Ilikuwa ni shangwe na furaha tupu kwa washiriki na ubunifu wao.
Mwakilishi wa Kagera, Jamia Abdul, akicheza ngoma ya Kihaya.
Mikogo pia ilipewa nafasi yake mbele ya meza kuu.
Rais wa Miss Utalii Tanzania na Jaji Mkuu wa kinyang’anyiro hicho, Gideon Chipungahero ‘Chipss’ (kulia) na majaji wenzake wakikusanya pointi.
Meya wa Manispaa ya Temeke, Maabad Hoja, akimvisha Sasha mrembo huyo baada ya kutangazwa mshindi.
DJ Max (kulia) na Mc Adria Cleophace walifanya kazi kubwa ya kunogesha tukio hilo. PICHA : RICHARD BUKOS / GPL

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...