Bomba linalotoa maji katika kisima cha kaloleni na hatimaye
kuunganishwa katika mtandao wa maji kwa ajili ya wakazi wa
Mabogini,Pasua na Bomambuzi.
Kaimu mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dk Ibrahim Msengi akiotesha mti
katika chanzo cha maji cha kaloleni wakati wa kilele cha maadhimisho
ya wiki ya maji iliyofanyika katika kata hiyo.
Mkurugenzi wa manispaa ya Moshi Bernrdette Kianabo akiotesha mti
katika chanzo cha maji cha Kaloleni wakati wa kilele cha maadhimisho
ya wiki ya maji iliyofanyika katika kata ya Kaloleni.
Mwenyekiti wa bodi ya mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingiara
mjini Moshi ,Sharry Raymond akiotesha mti katika chanzo cha maji cha
Kaloleni.
Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii ,Moshi
HALMASHAURI ya Manispaa ya Moshi imewatoa hofu wakazi wa kata za
Kaloleni, Pasua na Mabogini wanaotumia maji kutoka kisima cha Kaloleni
kwamba ni salama kwa matumizi ya nyumbani licha ya taarifa kuwa
yanaathiriwa na dampo lililopo jirani.
Wakizungumza katika kilele cha wiki ya maji,mkurugenzi wa
manispaa,Bernadette Kinabo na kaimu mkurugenzi wa mamlaka ya majisafi
na usafi wa mazingira Moshi (MUWSA),Isa Osena wamesema kisima hicho ni
kirefu na hupimwa kitaalamu kila mwezi.
Kauli hiyo ilifuatia kitendo cha wananchi wa kata hiyo,kumpokea kwa
mabango yenye ujumbe mbalimbali,kaimu mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Dk
Ibrahim Msengi wakilalamikia usalama wa maji hayo lakini pia kutopata
maji licha ya kisima kuwapo kwao.
Mwenyekiti wa mtaa wa Kaloleni,Ndama Bin Ndama,alisema wananchi hawana
imani na maji hayo kutokana na majitaka yanayochurizika kutoka katika
dampo kuu,lakini pia hawana maji licha ya kuwepo kisima eneo lao huku
wakilalamikia maji kupelekwa kata za jirani.
Katika majibu yao,Kinabo na Osena walisema kisima kina urefu wa mita
100 na hupimwa kila mara na dampo likiwa umbali wa zaidi ya mita 60
na limetengenezwa kitaalamu kwa kuwekewa msingi wa saruji inazozuia
maji kuelekea katika kisima.
Aidha Kinabo alisema MUWSA imetenga zaidi ya Sh Mil 236 kwa mwaka wa
fedha 2013/204 kwa ajili ya kuongeza vyanzo vipya huku manispaa
ikitarajia kuzindua mpango wa uoteshaji miti Mil 2 katika vyanzo na
makazi kuanzia April 10 hadi 16 mwaka huu.
Awali kaimu mkuu wa mkoa,Dk Msengi akizindua kisima cha Kaloleni
kilichoongeza uzalishaji wake kutoka lita za ujazo 71 kwa saa hadi
lita 1200 kwa siku na kukarabatiwa kwa Mil 41.2, alitaka wananchi
kukilinda na kuotesha miti kwa wingi.
Dk Msengi alisema hakuna sababu ya wananchi kuilaumu MUWSA au manispaa
kuhusu upungufu wa maji wakati wao hawajaotesha miti ambapo alielezea
mpango wa wilaya kutenga kila jumamosi ya mwezi kwa ajili ya usafi wa
mazingira na upandaji miti.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...