Na Shaffi Dauda


Hatimaye makamu mwenyekiti wa klabu ya Simba Godfrey Nyange Kaburu ametangaza rasmi kujiuzulu nafasi yake kwenye klabu ya Simba.

Taarifa rasmi kutoka kwenye uongozi wa Simba  ni kwamba Kaburu leo ametuma barua pepe kwenda kwa mwenyekiti wa klabu ya Simba Mh.Aden Rage akimuelezea maamuzi yake ya kujivua madaraka ya kuitumikia Simba kutokana mgawanyiko mkubwa uliopo kwenye uongozi wa klabu hiyo.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari Kaburu ameelezea kwamba kamati ya utendaji imegawanyika na ufa uliopo hautoi nafasi nzuri kwake kuitumikia vizuri Simba, akisema ni moja ya sababu ya timu yao ya Simba kutofanya vizuri katika michuano mbalimbali inayoshiriki.

Pia Kaburu amesema amechukua maamuzi hayo ni njia mojawapo ya kuwajibika kama kiongozi kutokana mambo kutokwenda vizuri hali ambayo imesabababisha kutukanwa na kupigiwa kelele nyingi na wanachama na wapenzi wa Simba SC Mwenyekiti. 


Hivyo ameamua kujiuzulu kupisha wanachama wengine wa Simba waweze kuliongoza jahazi la klabu hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. Maji ya shingo!!!

    Hapa ndio pale unaposhuhudia Punda anakaa chini baada ya kuelemewa na mzigo mgongoni!

    Duhhh huwezi amini na ngebe zake jamaa huyu mwenyewe anaachia ngazi?

    ReplyDelete
  2. Kaka kaburu nakupongeza sana tena sana kwa kuwa kama mtu umeshindwa kusimamia FAT mpaka mkafukuzwa je unaweza kuongoza hata familia yako?!

    ReplyDelete
  3. Jamani mm kama shabiki wa Simba mambo sio kwa kweli. Embu atoke tuone asijekuja mtu mwinngine mwenye kuleta mabadiliko lakini sisi waTZ tuko after money sana hatuangaliagi Future. Alafu maneno mengi ka Kasuku.

    ReplyDelete
  4. hapo hata kwa mangumi hakuna atakaye utaka uongozi wa msimbazi kwa sasa.

    uongozi umekuwa ni kasa wa sumu!

    ReplyDelete
  5. hapo hata kwa mangumi hakuna atakaye utaka uongozi wa msimbazi kwa sasa.

    uongozi umekuwa ni kasa wa sumu!

    ReplyDelete
  6. Ngoma inapokolea ni wakati Konga 'ngoma ndogo' zikirindima,,,na pale Msimbazi 'mibolo' imekolea Mabosi wa Timu wamechanganyikiwa mmoja baada ya mwingine wanaachia ngazi!

    ReplyDelete
  7. Karibu Yanga S.C tutakupa nafasi hiyohyio unayoiachia Msimbazi !!!

    Je, ukivua hilo gwanda jekundu na ukivaa Kijani na Njano utaota mkia?

    ReplyDelete
  8. Nenda zako Yanga!

    Pana uvumi unaosema uwa kwewe Kaburu ni mwana Jangwani!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...