Hii ngoma inaitwa Breakin' (There's No Stopping Us)lakini kina David V na mdau Mesiaki walikuwa wanaimba "Maiko Jekson njooo, sitaki kama hutaki nenda...." Ah! Raha tupu...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Haa haa,Ankal miaka hii ya '1980s'ilikuwa siyo kama sasa hivi ambapo unaweza kuingia online na kutafuta mashairi(Lyrics) ya wimbo fulani na kuyapata ili ufahamu mwanamuziki anaimba kitu gani.Sasa mambo yamekuwa rahisi,kuna TV zinapiga muziki saa 24,internet n.k Kwa hiyo tulikuwa tunaimba kila utakachofikiria kichwani na ndiyo maana juzi humu kuna mdau aliandika "Ankala naomba utuwekee na ule wimbo wa yeleleee komandoooo yelelee komandoooo"-Na kwa faida yake kama atarudi kwenye blog hii ule wimbo unaitwa IKATI(Paka-kwa Kizulu) uliimbwa na jitu la Miraba Minne Condry Ziqubu(1987?) album Skorokoro anaweza kuutafuta na kuupata,upo unapatikana

    David V

    ReplyDelete
  2. Ahahahahahahaaa haya ankal umegusa nyoyo za wengi sana kwa wimbo huu, hakika ya kale dhahabu , shukrani sana kutukumbusha enzi zetu, nakumbuka DJ wetu shuleni alikuwa Mkurugenzi wa sasa wa Clouds Radio Joe KUSAGA basi na changer wakati huo skuli , full shangwe.

    ReplyDelete
  3. Ahsante Madu David V. kwa kutoa Nondoz za wimbo huo!

    Ni mimi Mo Tzn ndiye niliomba hiyo yelele komandooo ,yelele Filipo kumbe Wimbo unaitwa 'Ikati' yaani Paka kwa Kizulu.

    Ndio faida yenyewe watu wana gallery za mambo mengi sana, ndio maana Wahenga walisema penye wengi hapaharibiki jambo, na ndio pana jamaa Madu mwenzetu aliona Maoni yanayozungumza kuhusu GMO (Genetically Modified Seeds)akasema kuwa Kilimo cha namna hiyo kina madhara, lakini akaacha kutoa taarifa za madhara yake, sasa hili ni jamvi la faida na sio jamvi la ubinafsi.

    Aisee Libeneke oyeeeeee!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...