WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema Serikali itaitisha kikao cha wadau mbalimbali kutoka taasisi za dini, mashirika yasiyo ya Kiserikali pamoja na vyama vya siasa ili kujadili mustakabali wa Taifa la Tanzania na hasa suala la amani na utulivu.
 
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana mchana (Jumatano, Machi 20, 2013) wakati wa mahojiano maalum na kituo cha Redio Vatican kilichopo Vatican City, mjini Roma, Italia.
 
“Serikali inatarajia kuitisha kikao cha wadau wote kutoka vyama vya siasa, mashirika ya dini, NGOs, ili kutafakari nini kifanyike ambacho kitasaidia kuendeleza amani na utulivu... tutaitisha kikao hiki tarehe 4 Aprili,” alisema Waziri Mkuu wakati akihojiwa na Padri Richard Mjigwa, Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...