Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL unawatangazia abiria wote na wananchi kwa jumla  kuwa treni kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza , KIgoma na Mpanda katika siku za Jumanne na Ijumaa utabadilika kutoka saa 8:30 mchana na kuwa saa 3:00 usiku kuanzia Aprili 02, 2013.



Aidha na kwa treni kutoka Mwanza kuja Tabora itaondoka saa 1:30 usiku na ile ya Kigoma kurudi  Tabora itaondoka 3:00 usiku. Mabadiliko haya yanatokana na  kuanza zoezi la utandikaji wa reli mpya kati ya Stesheni za Kitaraka (Singida) na Malongwe (Tabora)umbali wa kilomita 89, kazi ambayo itarajiwa kufanyika kwa saa 8 kila siku na hatimaye kukamilika baada ya miezi 6.



Uongozi wa TRL unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano kwa niaba ya  Mkurugenzi Mtendaji Mhandisi Kipallo Aman Kisamfu.


TRL Makao Makuu,

Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...