Ndugu  Michuzi,
 
Shirika la ndege la kisiwa cha  Samoa, Samoan airline wameanzisha utaratibu wa kulipia nauli ya ndege kulingana na uzito wa mtu na mizigo. Wenyewe wameiita ' Fare weight'  system.The lighter the passenger the lighter the fare. Yaani jinsi unavyokuwa  na uzito  mdogo  ndivyo unavyolipa   nauli ndogo. Utaratibu huu umeanza  kuanzia mwezi november mwaka jana na watu wamependezwa nao, hata wale  wenye  uzito mkubwa wameona  ni sahihi kufanya  hivyo, ingawa wanalipa  zaidi kuliko watu wenye  mzito mdogo. 
Watanzania mnaionaje hii kitu tukii copy & paste? Nadhani  ni jambo zuri ambalo vile vile linaweza kuchangia watu kuchunga  afya  zao  hasa swala la kuongeza  uzito bila mpango.
 
Mdau  Ruger
Ughaibuni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Yeeheee, Wasamoa ni watu walioshiba sana - hakuna mzaha, they are really huge people.

    ReplyDelete
  2. itasaidia watu kudhibiti vitambi aiseee naniii!

    ReplyDelete
  3. Mimba itakuwaje? Italipia tumbo pia

    ReplyDelete
  4. Jamaa wana hoja ya msingi kwa kuwa ndege ina limitation ya uzito!!

    ReplyDelete
  5. SUMATRA katika kupanga nauli za vyombo vya usafiri walitakiwa kufuata huu utaratibu wa kulipa kadri ya uzito wako.

    ReplyDelete
  6. Heee,

    Jamaa wakilijua Soko la Tanzania kwa kweli watapa utajiri mkubwa sana!

    Ni vile wa Tanzania tuna hulka mbaya ya kupenda kunenepeana na kufuga vitambi.

    ReplyDelete
  7. ohooo wamiliki wa Mabasi na Madaladala wa Bongo wakisikia hii mbona tutakoma?

    Utakuta wapiga Debe/Mateja na Makondakita wa Mabasi na mizani mlangoni mwa basi ili kuwapima uzito abiria kabla ya kupanda mabasi!

    ReplyDelete
  8. Mdau hapo juu mimba inatakiwa iwe exceptional otherwise wanawake tutasema tunabaguliwa na safari hii patachimbika - wanaume hakutakalika!

    Mdau - mama mwenye watoto wawili

    ReplyDelete
  9. Kwenye Dala ndiyo watoze kwa Usito na ukubwa wa makalio.

    ReplyDelete
  10. Mdau wa 3 hapo juu,

    Sula la Mimba ninaomba tusilijadili kwa kuwa kila mmoja wetu hapa lazima atakuwa amezaliwa na mama yake kwa njia ya mimba.

    Namuunga Mkono Mdau mama wa watoto wawili anony wa Thu Apr 04, 01:12:00 pm 2013

    TAFADHALI KWA SUALA LA MIMBA NA MAMA ZETU TUACHE KEBEHI NA DHARAU !

    ReplyDelete
  11. Wewe Mdau wa tatu unaeongela MIMBA akili zako nzuri kweli?

    Pana aliyeweza kuiona dunia bila kupitia ndani ya mimba?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...