Mtuhumiwa wa mauaji ya Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki parokia ya minara miwili mjini Zanzibar, Omar Mussa Makame (35) akiongozwa na Askari polisi kuingia katika Mahakama Kuu ya Zanzibar  kusikiliza kesi inayomkabili.
 wa Mauaji ya Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki parokia ya minara miwili mjini Zanzibar, Omar Mussa Makame (35) kulia akizungumza na mawakili wake Abdalla Juma kushoto na Rajab Abdalla muda mfupi baada ya kutajwa kwa kesi yake Mahakamani hapo. 
 Mawakili wanaomtetea Mtuhumiwa wa mauaji ya Padri , Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki parokia ya minara miwili mjini Zanzibar, Omar Mussa Makame (35) wakili Abdalla Juma (kulia) na Rajab Abdalla wakiwa mezani pao  kabla ya kutajwa kwa kesi ya mteja wao katika mahakama Kuu Vuga mjini Zanzibar
Mtuhumiwa wa Mauaji ya Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki parokia ya minara miwili mjini Zanzibar, Omar Mussa Makame (35) akiwa katika Mahakama Kuu ya Zanzibar kabla ya kesi yake kutajwa mahakamani hapo.
 Picha zote na Haroub Hussein

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 19 mpaka sasa

  1. KWA MTU KUPOTEZA UHAI, JE KUNA JAMBO LA KUFURAHISHA NA KUMFANYA YEYOTE -WHETHER NI MTUHUMIWA AMA ASIYE MTUHUMIWA- KUTABASAMU NAMNA HII? evil, evil, evil, SHAME ON YOU.

    ReplyDelete
  2. Tanzania kuna Amani kweli.jamaa hata havalishwi bullet proof akisindikizwa mahamani. na ana bonge la tabasamu Duuh.Waje huku wajione.
    Mdau USA

    ReplyDelete
  3. Jamani nimie peke yangu sijaelewa ama something is seriously wrong with this man? anachocheka ni nini? kuondoa uhai wa mtu yeyote duniani ni a very evil act and for him to seat there and smile as though he won a lottery is beyond me! shame on you! Mungu wako ndo atakaye kuuhukumu.

    ReplyDelete
  4. KUNA WATU WANAMAUZI KWELI,NAHIS HAKUTEGEMEWA KUSHIKWA

    ReplyDelete
  5. hivi huyu ndio anafanana na ile picha iliyochorwa "kitaalamu", nadhani tunahitaji kupima macho.

    ReplyDelete
  6. kesi ina utata kweli kweli hiyo, muwaji qa kweli yuko nje anakula kuku wacha tuyaone.

    ReplyDelete
  7. Kwa nini munamuhukumu kwamba yeye ni muuaji wakati hata kesi yenyewe haijaanza?

    Shame on you too!

    ReplyDelete
  8. Siyo tabasamu ya kawaida amechanganyikiwa Hutu kama kweli ni yeye ameua au la.

    ReplyDelete
  9. Munaoshangaa jamaa anavyotabasamu mlitaka alie? Kama hajahusika na hayo mauaji?
    Kwanini asiwacheke hao polisi kwa uchungizi mbovu wa kumkamata mtu sio

    Tena kwa usumbufu atakaopatiwa na kuitwa muuaji kabla hata ya hukumu kutoka hamuoni ni makosa?

    ReplyDelete
  10. hivi watz wenzangu wapi mwaenda mtu anafanishwa na mtuhumiwa wa mahuaji ya padri tayari mmehukumu tayari kwani tuhuma ni chanzo cha kupata ukweli.

    ReplyDelete
  11. Ni vizuri tukavuta subira kwakua huyu bado ni mtuhumiwa hakuna haja ya kumlaani kabla hajatiwa hatiani, nadhani picha halisi inaonekana hata yeye mwenyewe hana shaka kua atapangua kikamilifu tuhuma dhidi yake.

    ReplyDelete
  12. Watu wapo US wengine UK humu ndani hawajui nini maana ya MUUAJI na MTUHUMIWA,
    Hivi nyie kuna aliemuona huyu kaua,kwa taarifa yenu Mwendesha mashtaka ametupilia mbali ushahidi wa uongo aloutoa kamishna na timu yake yote

    na amewambia wamuachie huyu jamaa wakamtafute Muuaji,kwanza masaa 24 yamepita sheria huyu hana kesi hata kama auwe,
    Huyu jamaa kilichomponza ni ile kauli yake alipotoa maoni yake katika kongamano la katiba kuwa Watu wakichoka basi wataingiza silaha kupambana,
    Polisi wameshindwa kumpata mtu wameona bora wamkamate huyu,Shame on you mlotoa maoni kulinganisha Mtuhumiwa na Muuaji,

    ReplyDelete
  13. he has the right to smile or even laugh because he's innocent until proven guilty. do they have a concrete evidence to connect him with the murder? "no". To be honest, i do not believe evidence based on eye witness, its always not accurate.

    ReplyDelete
  14. Watu wengine wapuuzi sana hasa watanzania wanapenda kuchonga sana. Huyu jamaa awe mtuhumiwa au muuaji anacho smile ni nini???? Maoni ya watu wengine hapa yanaonyesha jinsi gani tuna akili finyu. Hata kama wewe sio muuaji kinachokufurahisha ni nini unapotuhumiwa kwa mauaji???

    ReplyDelete
  15. TABASAMU LA NGUVU BILA WASIWASI WOWOTE, HADI RAHA ... MTU UKIWA UMESINGIZIWA KESI HAMNA CHA KUOGOPA, ANAYEOGOPA NI YULE MWENYE MAKOSA. KWANZA KESI YENYEWE INAONEKANA ANAUNDIWA TU BAADA YA KUKOSEKANA MHALIFU WA KWELI. POLISI WA BONGO NA FBI WAO WANAONEKANA NI WABABAISHAJI TU.

    ReplyDelete
  16. hapa ninachokiona ni Watanzania wengi tunakurupuka, hata ukiangalia haya maoni, kwa nini asitabasamu wakati anajuwa kuwa police wamechemsha na ndio maana DPP ameshawarushia jalada lao na kamwambia Kamishna Mussa wakamtafute muuwaji kuwa huyu hahusiki na mauaji ila nyinyi munakurupuka eti alie, alilie nini wakati ana uhakika keshatolewa kwenye orodha ya wauwaji, police wanachokifanya ni kutapatapa tu wakifkiria pressure ya kanisa huku mtuhumiwa hawajampata juu ya kuletea mpaka FBI

    ReplyDelete
  17. Duh Maajabu

    ReplyDelete
  18. Nakupenda Tanzania

    ReplyDelete
  19. kwa wasiomjuwa, kutabasamu kwa huyu swahiba ndio kawaida yake na ndio maisha yake kama alivyo Kikwete.Undani zaidi mungu ndie ajuwae na ndio atakae muongoza.

    msimuhukumu mtu asie na hatia kwani bado ni mtuhumiwa. sio kila endae jela wote wana hatia huwa ni wapita njia. kunakutendewa haki ama batili yote ma2 yanawezekana.

    Mola amsaidie kijana huyu.kwani situnakumbuka yale ya Lulu dhidi ya kanumba."TUTENDEANE HAKI WANADAMU DUNIA TUNAPITA".Wasia wangu kwenu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...