Kwa niaba ya watanzania wote wanaoishi katika mji wa Guangzhou china tunapenda kuwataarifu kwamba tumeshitushwa na kuhuzunishwa sana na taarifa za vifo vya ndugu zetu vilivyotokea kwa kudongokewa na ghofofa.
Jumuiya kwa niaba ya watanzania wote nchini China, tunatoa pole kwa wahanga wote, aidha tunawatakia watanzania wote pamoja na ndugu jamaa na marafiki wote wawa wafiwa moyo wa subira katika wakati huu wa majonzi.
Tunaomba mwenyezi Mungu azipumzishe mahala pema peponi roho za marehemu wote, tuko pamoja na familia za marehemu wote katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
Mwenyezi Mungu Azilaze roho za marehemu wote mahali pema peponi
Amen.
Imetolewa na
Jumuiya ya Watanzania wanaoishi Guangzhou China.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...