Balozi wa Tanzania nchini China Philip Marmo akiongea na mwekezaji Zhou Yi (wa pili kushoto) ofisini kwake jijini Beijing China. Wengine katika picha ni Pan Lei, Mkurugenzi wa Kampuni ya kichina ya Fashion Tourism yenye ofisi yake nchini pamoja na Allen Lee kutoka Chama cha Mawakala wa Utalii Beijing, China. (Picha na Pascal Shelutete wa TANAPA)
Mwekezaji wa China Zhou Yi 

Na Pascal Shelutete
Milionea wa kutoka Jamhuri ya Watu wa China Zhou Yi anatarajia kujenga loji kubwa ya kisasa katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Zhou alisema hayo jana jijini Beijing nchini china alipokutana na ujumbe wa serikali ya Tanzania unaotembelea China kwa lengo la kutangaza utalii na kutafuta wawekezaji katika sekta ya utalii nchini.
Zhou anamiliki mtandao wa makampuni tanzu yanayofahamika kama Hengxu Group of Companies yenye makao makuu yake katika mji wa viwanda wa Sichuan na ameajiri watu zaidi ya 7,000 na ana mtaji wa zaidi ya dola za kimarekani milioni mia saba alisema kuwa alitembelea hifadhi ya Serengeti mwezi Machi mwaka huu na kuvutiwa sana  na uzuri wa uasili uliopo Serengeti.
Alisema kuwa hivi sasa yuko katika hatua za awali ya kuomba kupatiwa eneo la kuwekeza ambapo ujumbe wa serikali unaoongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Bi. Nuru Millao ulimuhakikishia upatikanaji wa eneo hilo ili kupunguza tatizo la uhaba wa vitanda kwa wageni nchini.
Ujumbe wa Tanzania uko nchini China kuhudhuria maonyesho maarufu ya utalii ya COTMM katika jiji la Beijing pamoja na kuandaa semina kwa wawekezaji wa China na Wamiliki wa kampuni za Utalii kuhusu vivutio vya utalii nchini pamoja na kuainisha fursa zilizopo za uwekezaji katika sekta ya utalii nchini. Semina hizi zinazofanyika katika miji ya Shanghai, Beijing na Guangzhou zinalenga kuongeza idadi ya watalii na wawekezaji kutoka China nchini.
Jijini Beijing emina hizi ilivutia idadi kubwa ya wawekezaji ambao walihamasika hasa kutokana na fursa zilizopo katika maeneo yaliyohifadhiwa nchini. Wengi waliamua kutembelea Tanzania kaika siku za usoni ili kuona maeneo watakayoamua kuwekeza.
Mapema Balozi wa Tanzania nchini China na Bi. Millao waliwahakikishia washiriki kuwa Tanzania ni eneo zuri kuwekeza kwa sasa hasa kwa kuwa na vivutio vingi ikiwa ni nchi ya pili duniani baada ya Brazil. Aidha, wawekezaji hao walihamasishwa kuchangamkia fursa zilizopo hasa kutokana na utulivu wa amani uliopo nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Sio mbaya lakini hao jamaa siwaamini kabisa ...wanapenda sana kula wanyama mbalimbali....msije mkastuka mbuga nye

    ReplyDelete
  2. I think that is a very wrong approach. The bed capacity within Serengeti ecosystem is more than enough unless we want to spoil "the goose that lays the golden eggs" and engage in mass tourism like our neighbors in the north. Such ivestments should be directed to Katavi National Park for diversification and opening up other new tourism products. We should put to maximum use the Songwe International Airport in Mbeya as the hub to SADC region and link to Mpanda as well as Copper belt in Zambia. I am proposing a tourist circutit linking Nsumbu National Park on Lake Tanganyika shores in Zambia to Mahale, Katavi, Kitulo and Ruaha national parks. The market is unexplored and that is where the Chinese investments should be directed.

    ReplyDelete
  3. Hapo ni kumkabidhi panga mwendawazimu..wachina wanatumia pembe za ndovu na pembe za rhino na mifupa ya chui kama dawa...si mmempa shamba huyo akavune. tunahitaji wawekezaji lakini sharti tuangalie na sifa za wawekezaji sio hela tu...

    ReplyDelete
  4. The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!
    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    The Chinese have arrived in Serengeti!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...