Mwakilishi wa Jimbo la Makunduchi Zanzibar, Mhe Haroun Ali Suleiman,akimkabidhi fedha taslima zaidi ya  shilingi Milioni tatu, mmoja wa viongozi wa shehia ya Mzuri kwa ajili ya mashindano ya kumuenzi aliyekuwa kiongozi wa siku nyingi nchini marehemu Hasnou Makame


 Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi naUshirika Mhe Haroun Ali Suleiman akizungumza na Balozi mdogo wa India hapa nchini Mhe Pawal Kumar ofisini kwakwe Mwanakwerekwe mjini Zanzibar, jinsi India itakavyoweza kuisaidia Zanzibar juu ya kuanzishwa kwa Benki ya Jamii.

Wanahabari  wa vyombo mbalimbali vya habari wakipata maelezo kwa Mshauri Mkuu wa Msafara wa wakandarasi kutoka India Bw. Ummashan Kar Misra juu ya kukifanyia matengenezo kiwanda cha sukari Mahonda 
Mfanyakazi wa Idara ya Usafiri barabarani (kushoto) kwa kushirikiana na Askari wa Usalama barabarani wakiwa katika operesheni ya kukagua vyombo vya moto barabani katika kuadhimisha wiki ya usalama barabarani 

Kondakta wa gari ya abiria ya Chwaka akiondoa marembo ya mbele ambayo yanamzua dereva kuona mbele baada ya kuamriwa kufanya hivyo na Askari wa Usalama Barabarani katika uperesheni wa ukaguzi wa Magari ulioandaliwa na Idara ya Usafiri na Lesseni kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya usalama barabarani. 
Picha zote na Khamisuu Abdallah wa Globu ya Jamii, Unguja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. tofauti ya bara na zanzibar, zanzibar umekosea unapewa nafasi ya kurekebisha kosa, bara umekosea unapigwa faini, mradi umewalipa pesa yao hata usiporekebisha kosa haiwahusu

    ReplyDelete
  2. Ni vema mmeliona hilo kwani hata mimi nipandapo basi huwa nakerwa sana na hayo mapambo mengi kwenye kioo cha dereva ambayo humzuia hata dereva sione mbele vizuri

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...