Pichani na sehemu ya raia wakiwamo wanawake, watoto na wanaume wakikimbia machafuko katika eneo la Mashariki ya Kongo, siku ya Jumatano, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, lilikuwa na majadiliano ya siku nzima kuhusu ajenda ya Wanawake, Amani na Usalama. Katika Majadiliano hayo, ilidhihirisha wazi kwamba licha ya juhudi mbalimbali ambazo zimekuwa zikichukuliwa na Jumuiya ya Kimataifa katika kupigania na kutetea haki na usalama wa wanawake katika maeneo yenye vita, bado wanawake, watoto na hata wanaume, wanaendelea kudhurumiwa utu na hadhi yao kwa kufanyiwa ukatili mkubwa ikiwa ni pamoja na kubakwa, mbinu inayoendelea kutumiwa kama mbinu ya kivita. Ukatolewa wito wakati wa majadiliano hayo wa kuendelea kuwachukulia hatua za kisheria wale wote wanaobainika kuhusika na ukatili huo ikiwa ni pamoja na kutafuta namna ya kuwafidia waliodhulumiwa utu wao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...