Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya Diwani Athuman ............................................................. Taarifa kutoka Tunduma mkoani Mbeya zinadai kuwa hali si shwari katika eneo hilo kutokana na kuzuka kwa vurugu kubwa zinazodaiwa kusababishwa na masuala ya kiimani ya nani achinje kati ya mkristo na Muislam . Habari zinasema vurugu hizo zimeanza majira ya saa nne asubuhi kwa makundi ya vijana kuandamana mitaani na kuvutana kuhusu uamuzi wa viongozi wa dini ya kikristo Tunduma kuandika barua kwa mkuu wa wilaya kutaka kuruhusiwa kuchinja wakati wa Pasaka. Insemekana kuwa kabla ya Ijumaa kuu viongozi hao wa dini ya Kikristo walikutana na mkuu wa wilaya Mhe. Momba Abuud Saidea ambae aliwataka kuwasilisha barua rasmi ya kufanya hivyo . Hata hivyo inaelezwa kuwa vurugu hizo za leo hazina mahusiamo ya moja kwa moja na masuala ya dini kwani wanaoshiriki katika vurugu hizo ni vijana wapiga debe ambao baadhi yao wamechanganyika na vibaka kwa lengo la kuchafua hali ya hewa, kwani suala la uchinjaji ambalo lilifanyika siku ya Pasaka halikuwa na mvutano wowote baada ya wakristo kuchinja katika bucha zao na waislamu hao kuchinja katika mabucha yao na kila mmoja kufanya biashara kwa kupata wateja wake kama kawaida . Ila katika hali ya kushangaza ni baada ya leo kuibuka kundi hilo la vijana wanaofanya kazi katika stendi na vijiwe mbali mbali kuanzisha vurugu kiasi cha polisi kuingilia kati kwa kutumia mabomu ya machozi na kuwatawanya wananchi waliokuwa wamekusanyika maeneo mbali mbali . Kutokana na vurugu hizo mpaka wa Tunduma ambao unaingia nchi za kusini wa Tanzania ulifungwa pamoja na magari yaliyokuwa yakitoka Sumbawanga pia kuzuiwa kuendelea na safari hadi hali hiyo ilipotulia mida hii saa 8 mchana baada ya kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya Diwani Athuman kufika eneo hilo. |
Home
Unlabelled
VURUGU ZAIBUKA TUNDUMA LEO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Sisi wakristo aka wamisionari,nikiwa mdogo wazazi wakinunua kitoweo cha kuku, au wakati wa pasaka au noeli mbuzi, basi jirani yetu muislamu aka mwana zuoni,tutamuomba aje kuchinja, kwani sisi tulikuwa hatuna noma, sababu washikaji zangu kina abdallah, athumani, shabani wanaweza nao kuzuka nyumbani baada ya kucheza cha ndimu ili wapate "MMANGO" sote tukamanga, sikuhizi vurugu tupu, upendo wa zamani umeishia wapi?
ReplyDeleteupendo wame na wanauondoa wao! ni bahati mbaya sana kwamba badala ya kuendelea kuwapenda na kuwavumilia, na sisi tunajifunza kuwa kama wao!!
ReplyDeletekwa nini wasiruhusiwe kuchinja?
ReplyDeleteuzuri ni uwazi, kutakuwa hakuna kula kwenye nyumba za dini nyengine iwe harusi, kilio, au laa.
upendo wameondoa CHADEMA na baadhi ya viongozi wa dini wanaochochea fujo
ReplyDeleteSwala la nyama linahitaji busara isiyo ya kawaida.Hili linaweza kulipua nchi katika vipande vipande maana linagusa imani zetu.Wakristo hawana shida kula nyama iliyochinjwa na waislam/wasio na dini au wakristo wenzao tatizo hilo halipo.Tatizo lipo kwa waislam ambao pamoja na mambo mengine wao wanawaona wakristo kama "makafri" hawafai kuchinja nyama si kwasababu nyingine yoyote bali kwasbabu mafundisho yao wanavyodai kuwa ni makafri" na kwa wakristo wana haki sawa kama wengine na uwezo wa kuchinja wanao sasa hapa ndipo biashara inaponoga.Mkuu wa kaya hana maamuzi amebaki maneno matupu.sasa sijui
ReplyDeletewana "filosofia" walisema YOU CAN FOOL SOME PEOPLE SOME TIME, BUT CAN'T FOOL THE PEOPLE ALL THE TIME. Kwa maana hiyo, kizazi cha sasa kila upande umegundua hilo lakini kuna upande mmoja ambao umedhulumiwa zaidi, na ule uliodhulumu unajitahidi kupata mashiko ya kuendelea kuhakikisha unaendeleza dhuluma za tangu mwanzo. KUMBUKENI kizazi kipya hakijua habari ya kuvumiliana. SERIKALI IKIKAA KUSHUHULIKIA UPANDE MMOJA KWA VITENDO NA MWINGINE KWA MANENO, Basi tunaelekea tutafuta kuheshimiana kwa STYLE ya Rwanda 1994. na safari hiyo ya rwanda imeanza basi ndio tumeondoka ubungo kuitafuta Dom, Sgd, kahama Kagera kabla ya kufika KIGALI. WATANZANIA WA SASA TUMESHAPOTEZA MAMBO 3. UPENDO, KUSHIRIKIANA NA KUVUMILIANA. na kwa sehemu kubwa serikali imechangia kwa kukumbatia UPANDE mmoja
ReplyDeletedemokrasia!!
ReplyDelete